Na Mathias Canal, Pemba

Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Ndg Shaka Hamdu Shaka amehitimisha ziara ya siku nne ya kikazi Kisiwani Pemba-Zanzibar kwa kuzuru katika Mikoa yote miwili ya Kusini Pemba na Kaskazini Pemba na Wilaya zake zote za Wete, Mkoani, Chakechake na Micheweni.

Katika ziara hiyo pamoja na mambo mengi alikagua na kushiriki kufanya kazi za kijamii ikiwa ni pamoja na kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM 2015-2020, kushiriki kuona shughuli mbali mbali za uzalishaji Mali kupitia makundi ya vijana na kuwasaidia kwa kuwaunga mkono ili kuongeza mtaji wa miradi yao.

Alitumia ziara hiyo kuzungumza na makundi ya vijana kwa nyakati tofauti, viongozi wa CCM, jumuiya za CCM Pamoja na kushiriki shughuli zingine mbalimbali za kijamii, kiuchumi na kisiasa na kuwaasa kukaa maskani pekee pasina kufanya kazi za uzalishaji mali jambo ambalo litapeleka mbele maendeleo katika jamii.

Katika maeneo yote aliyozuru Kaimu Katibu Mkuu huyo alitilia zaidi msisitizo kwa vijana kujiunga na vikundi mbalimbali vya kijamii ili kupatiwa mikopo ya vijana inayotolewa na serikali kwa asilimia 5 kila mwezi.
Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Ndg Shaka Hamdu Shaka akiagana na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi mara baada ya kumaliza ziara ya siku nne ya kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi Visiwani Pemba.
Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Ndg Shaka Hamdu Shaka akiagana na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi mara baada ya kumaliza ziara ya siku nne ya kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi Visiwani Pemba. 
Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Ndg Shaka Hamdu Shaka akiagana na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi mara baada ya kumaliza ziara ya siku nne ya kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi Visiwani Pemba. 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...