Waziri wa Nchi anayeshughulikia Masuala ya Afrika kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Uingereza, Mhe. Stewart Rory atafanya ziara ya kikazi ya siku mbili nchini tarehe 22 na 23 Agosti 2017. 

Mhe. Rory anakuja nchini kwa madhumuni ya kutembelea miradi mbalimbali inayofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Uingereza (Department for International Development – DFID).

Aidha, wakati wa ziara hiyo, Mhe. Waziri Rory amepangiwa miadi ya kuonana na Viongozi wa Serikali akiwemo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb).

Baadhi ya miradi ambayo, Mhe. Waziri ataitembelea ni upanuzi wa Bandari ya Dar Es Salaam, Shule ya Msingi Mkoani, Bonde la Mto Msimbazi, Kiwanda cha Nguo cha Tooku kilichopo katika Eneo la Viwanda la Benjamin Mkapa, Mabibo jijini Dar es Salaam na kampuni ya Songas. 

Waziri Rory pia anatarajiwa kushiriki chakula cha mchana na vijana wa Kitanzania katika moja ya migahawa `ya kawaida katika mitaa ya jiji la Dar Es Salaam

Baada ya kukamilisha ziara yake, Waziri Rory ataondoka nchini tarehe 23 Agosti 2017 kurejea London. 


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, 

Dar es Salaam, 21 Agosti 2017

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...