Na David John Mwanza

 KADA wa   Chama cha Mapinduzi na Mwenyekiti Mstaafu wa Serikali  ya Mtaa wa kiloleli B Jijini Mwanza Joshua Mnana amesema kazi nzuri inayofanywa na Serikali inasababisha kukimarisha Chama  cha Mapinduzi CCM.
Mwenyekiti huyo mstaafu alisema kwamba hivi Sasa Makada na wanachama wa CCM wanatembea kwa kujidai na hiyo nikutokana na serikali iliyopo madarakani inafanya  vizuri ukilinganisha na huko nyuma.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Jijini hapa Mnana alisema hata kuhairishwa kwa baadhi ya Chaguzi ambazo zinaendelea kufanyika ndani ya Chama hicho niwazi kwamba hivi watu wanakipenda chama hivyo yeye haoni Kama kasoro.
 "Unajuwa ndugu waandishi zamani kulikuwa hakuna hiyo hali nasababu ilikuwa wanachama walikuwa wanashindwa kuchukua hata fomu ya kugombea kutokana na chama kilivyokuwa."alisema Mnana
  Aliongeza kuwa kuingia madarakani kwa serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt.John Magufuli kumefanya watu kukubali kazi zinazofanyika na kurudisha imani kubwa kwa Chama cha Mapinduzi.
Aidha akizungumzia mtaa wake wa kiloleli alisema kihalisia eneo hilo ni la milima lakini chini ya uongozi wa Rais Magufuli hivi wamepata barabara ya kiwango cha lami ambayo pia zimewekwa na taa nakufanya eneo hilo kuwa tofauti na mitaa mingine mkoani Mwanza.
  Pia Mnana aliomba viongozi wa eneo hilo ambao wapo madarakani hivi sasa kufanya utaratibu ili barabara izinduliwe na Rais Dkt Magufuli huku akiipongeza Kampuni ya Nyanza Road kwa kazi nzuri ya ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha juu.
  "Binafsi nitaendelea kuwa Mwanachama mwadilifu wa Chama cha Mapinduzi ccm na naunga mkono kwa asilimia mia moja kazi nzuri inayofanywa na rais Magufuli. "alisema Mnana

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...