Mwakilishi wa Zantel-Tanga Mansoor Ally, (kulia) akikabidhi mbuzi kwa kituo cha kulea watoto yatima cha Goodwill & Humanity Foundation kilichopo jijini Tanga wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika kituo hicho, siku ya Alhamisi ya wiki iliyopita ikiwa ni moja ya hatua ya kujitolea kwa jamii kwa Kampuni hiyo. Zaidi ya mbuzi 100 walitolewa katika mikoa mbalimbali ya bara na visiwani katika kuadhimisha sikukuu ya Eid Al Adha.
Meneja wa Data na Vifaa vya Intaneti, Hamza Zuheri (kushoto) akikabidhi mbuzi kwa mwakilishi wa kituo cha kulea watoto yatima cha Malaika kilichopo Kinondoni Malongwe jijini Dar, wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika makao makuu ya ofisi za Zantel jijini Dar es salaam, siku ya Alhamisi ya wiki iliyopita ikiwa ni moja ya hatua ya kujitolea kwa jamii kwa Kampuni hiyo. Zaidi ya mbuzi 100 walitolewa katika mikoa mbalimbali ya bara na visiwani katika kuadhimisha sikukuu ya Eid Al Adha.
Afisa wa Zantel Abdallah Saadun (kushoto) akikabidhi mbuzi kwa Afisa rasilimali watu wa kituo cha kulea watoto yatima cha SOS-Zanzibar, Bw. Salum Abdallah Salum (wa pili kushoto) wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika ofisi kuu ya Zantel iliyopo Unguja, siku ya Alhamisi ya wiki iliyopita ikiwa ni moja ya hatua ya kujitolea kwa jamii kwa Kampuni hiyo ambapo zaidi ya mbuzi 100 walitolewa katika mikoa mbalimbali ya bara na visiwani katika kuadhimisha sikukuu ya Eid Al Adha.
Afisa wa Zantel Abdallah Saadun akikabidhi mbuzi kwa walezi na watoto wa kituo cha kulea watoto yatima cha Mazizini-Zanzibar wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika ofisi kuu ya Zantel iliyopo Unguja, siku ya Alhamisi ya wiki iliyopita ikiwa ni moja ya hatua ya kujitolea kwa jamii kwa Kampuni hiyo ambapo zaidi ya mbuzi 100 walitolewa katika mikoa mbalimbali ya bara na visiwani katika kuadhimisha sikukuu ya Eid Al Adha. Anayeshuhudia kushoto ni Meneja Chapa na Mawasiiano wa Zantel, Rukia Mtingwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...