Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Hassan Simba Yahya akizungumza wakati wa Ufunguzi wa Kikao cha Wadau wa Usalama Barabarani, kinachojadili mabadiliko ya Sheria ya Usalama Barabarani. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa wizara, Joyce Momburi na Kushoto ni Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Polisi, Japhet Lusingu.Kikao hicho kinafanyika katika Ukumbi wa Bwalo la Polisi, Oysterbay, Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Joyce Momburi, akizungumza na wadau mbalimbali wa Usalama Barabarani (hawapo pichani), wakati wa Ufunguzi wa Kikao cha Wadau wa Usalama Barabarani, kinachojadili mabadiliko ya Sheria ya Usalama Barabarani. Wengine ni Kamishna Msaidizi, Japhet Lusingu (kulia), Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Balozi Hassan Simba Yahya (watatu kulia) na Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Polisi, Theopista Mallya. Kikao hicho kinafanyika katika Ukumbi wa Bwalo la Polisi, Oysterbay, Dar es Salaam.
Mwanasheria wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Mrakibu Msaidizi wa Polisi, Deus Sokoni, akisoma vifungu vya Sheria ya Usalama Barabarani mbele ya wadau mbalimbali wa Usalama Barabarani (hawapo pichani), wakati wa Ufunguzi wa Kikao cha Wadau wa Usalama Barabarani, kinachojadili mabadiliko ya Sheria ya Usalama Barabarani. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Joyce Momburi na kushoto ni Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Polisi, Theopista Mallya.Kikao hicho kinafanyika katika Ukumbi wa Bwalo la Polisi, Oysterbay, Dar es Salaam.
Mdau wa Usalama Barabarani, Henry Bantu, akitoa Historia ya Baraza la Usalama Barabarani wakati Kikao cha Wadau wa Usalama Barabarani, kinachojadili mabadiliko ya Sheria ya Usalama Barabarani.Kikao hicho kinafanyika katika Ukumbi wa Bwalo la Polisi, Oysterbay, Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...