Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Hassan
Simba Yahya akizungumza wakati wa Ufunguzi wa Kikao cha Wadau wa Usalama
Barabarani, kinachojadili mabadiliko ya Sheria ya Usalama Barabarani. Kulia ni
Kaimu Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa wizara, Joyce Momburi na Kushoto ni
Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Polisi, Japhet Lusingu.Kikao hicho kinafanyika
katika Ukumbi wa Bwalo la Polisi, Oysterbay, Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,
Joyce Momburi, akizungumza na wadau mbalimbali wa Usalama Barabarani
(hawapo pichani), wakati wa Ufunguzi wa Kikao cha Wadau wa Usalama
Barabarani, kinachojadili mabadiliko ya Sheria ya Usalama Barabarani. Wengine
ni Kamishna Msaidizi, Japhet Lusingu (kulia), Naibu Katibu Mkuu wa wizara
hiyo, Balozi Hassan Simba Yahya (watatu kulia) na Kamishna Msaidizi wa Jeshi la
Polisi, Theopista Mallya. Kikao hicho kinafanyika katika Ukumbi wa Bwalo la
Polisi, Oysterbay, Dar es Salaam.
Mwanasheria wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Mrakibu Msaidizi wa
Polisi, Deus Sokoni, akisoma vifungu vya Sheria ya Usalama Barabarani mbele ya
wadau mbalimbali wa Usalama Barabarani (hawapo pichani), wakati wa Ufunguzi
wa Kikao cha Wadau wa Usalama Barabarani, kinachojadili mabadiliko ya Sheria
ya Usalama Barabarani. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Joyce Momburi na kushoto ni Kamishna
Msaidizi wa Jeshi la Polisi, Theopista Mallya.Kikao hicho kinafanyika katika
Ukumbi wa Bwalo la Polisi, Oysterbay, Dar es Salaam.
Mdau wa Usalama Barabarani, Henry Bantu, akitoa Historia ya Baraza la Usalama
Barabarani wakati Kikao cha Wadau wa Usalama Barabarani, kinachojadili
mabadiliko ya Sheria ya Usalama Barabarani.Kikao hicho kinafanyika katika
Ukumbi wa Bwalo la Polisi, Oysterbay, Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...