Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
CHAMA cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mkuranga kimepata viongozi wapya wataongoza chama hicho kwa kipindi cha miaka mitano katika uchaguzi uliofanyika jana.

Katika nafasi ya Mwenyekiti Wilaya imechukuliwa na Ally Msikamo kwa kura 749 baada ya kuwashinda wagombea wawili , Abdallah Kihato kura 189 na Mbaraka Mahanaka kura 44.

Nafasi ya katibu Mwenezi Wilaya imechuliwa na Ben Mkulia kwa kura 89 na kuwabwaga wagombea wawili , Mchowi aliyepata kula 22 na Ali Ngalema kula Saba (7).

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Wilaya Mkuranga , Ali Msikamo amesema kuwa uchaguzi umeisha na kilechobaki ni kufanya kazi katika ya kuendesha chama katika kumsaidia Rais Dk. John Pombe Magufuli.

Amesema kazi ya chama kazi ya chama wilaya kuishauri serikali katika kusaidia chama kuendelea kushika dola ikiwemo na maandalizi ya uchaguzi mkuu.

Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega amesema kuwa uteuzi wa Naibu Waziri umetokana na wananchi wa Mkuranga na sio ujanja wake mwenyewe ndio uliomfanya aonekane.

Amesema kuwa maendeleo ya Chama na Utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi kuandaliwa mkutano utaohusisha wajumbe wote kuangalia walikotoka na wanako elekea.
 Mbunge wa Mkuranga , Abdallah Ulega alieapishwa leo kuwa Naibu Waziri wa Uvuvi na Mifugo, akizungumza katika mkutano mkuu wa uchaguzi wa Wilaya ya Mkuranga.

 Mwenyekiti mpya wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mkuranga, Ali Msikamo akiwashukuru wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Wilaya  kwa kumpa ridhaa ya kuongoza chama hicho kwa kipindi cha miaka miatano.
 Sehemu ya viongozi wa Mkutano Mkuu wa Uchaguzi.

Picha mbalimbali za uchaguzi Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga
Picha zote na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...