Msanii wa Bongo Fleva nchini IzzoBiznes akiimba na Mashabiki wa Tamasha la Efm Mziki Mnene katika Bar ya Dunda Dunda Bagamoyo.


Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii


MSANII wa muziki wa Bongofleva kutoka mkoa wa Mbeya Izzo Biznes amevunja mwiko kwa wakazi wa mkoa wa pwani kwa kuimba pamoja nao muziki wa Rap.

Izzo ambaye alipanda katika jukwaa la Mziki Mnene la Efm akiongozwa na RDJ Black ambaye alianza kumpigia wimbo wake unaokwenda kwa jina la Ridhiwani ongea na Mshua jambo lililokonga nyoyo za wakazi hao.

IzzoBiznes mbali ya wimbo huo aliwapagawisha wakazi hao kwa wimbo wake wa Shemeji ambao uliweza kuinua watu wote ambao walikuwa wamekaa katika viti na kuanza kuimba nae pamoja.

Baada ya wimbo huo aliongeza kibao chake kinachokwenda kwa jina la Kama Kijana ambao nao uliweza kuinua vijana wote wa Bagamoyo ambao waliimba nae pamoja.Mwisho alimaliza kwa kuimba free Style na kuunganisha wimbo wake wa Tumhoghele.
Msanii wa Bongo Fleva nchini IzzoBiznes akiimba na Mashabiki wa Tamasha la Efm Mziki Mnene katika Bar ya Dunda Dunda Bagamoyo.
Msanii wa Bongo Fleva nchini IzzoBiznes akiimba na Mashabiki wa Tamasha la Efm Mziki Mnene katika Bar ya Dunda Dunda Bagamoyo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...