NAIBU Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo amefanya ziara leo ya kukagua utekeleza wa maagizo ya serikali aliyoyatoa hivi karibuni katika Kituo cha Afya Makole Manispaa ya Dodoma.

Pamoja na maagizo mengine, Jafo aliagiza kuhakikisha kituo hicho kinafunga mfumo wa kielektroniki wa ukusanyaji mapato.

Akiwa katika ziara yake leo, Jafo amepongeza ufungaji wa mfumo huo huku akiwataka kuhakikisha wanaziba mianya ya upotevu wa mapato kwa kuwa hali ya ukusanyaji bado hairidhishi.

Amesema kwa mujibu wa taarifa aliyoipata kituo hicho kabla ya mfumo kilikuwa kikikusanya Sh.Milioni nne lakini kwasasa kinakusanya hadi Sh.Milioni 9.9 kwa mwezi jambo ambalo linaonesha bado kuna mianya ya upotevu wa mapato.

“Nawapongeza kwa kutekeleza maagizo ya serikali kwa kufunga huu mfumo lakini sijaridhishwa na ukusanyaji mapato wa kiwango hichi, kuna vituo vinakusanya hadi Sh.Milioni 24 nyie mnakusanya hivi bado haitoshi hakikisheni mnaziba mianya,”amesema Jafo
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akisisitiza jambo alipokuwa akikagua mfumo wa kielektroniki katika Kituo cha Afya Makole Manispaa ya Dodoma.
Wagonjwa wakiwa katika dirisha la malipo kwenye kituo cha Afya Makole Manispaa ya Dodoma.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akisalimia wagonjwa alipokuwa akikagua kituo cha Afya Makole Manispaa ya Dodoma.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...