Na Fredy Mgunda,Mufindi
Chama cha walimu wa Tanzania (CWT) wilaya
ya Mufindi mkoani Iringa kimemuomba mkurugenzi kuwakopesha viwanja walimu ili
kujikwamuamua na mazingira magumu wanayokumbana katika nyumba wanazoishi.
Hayo yalisemwa na mwenyekiti chama
cha walimu wa Tanzania (CWT) wilaya ya Mufindi Obi Kimbale alisema kuwa walimu
wamekuwa wakiishi katika nyumba chakavu au mbali na mazingira ya shule kitu
kinachosababisha kushuka kwa uwezo wa walimu kufundisha.
Kimbale alisema kuwa walimu hawana
pesa za kununua moja kwa moja viwanja hivyo kwa njia ya kuwakopesha inawezekana
kutokana kuwa ni waajiliwa wa serikali na mishahara yao inajulikana na ni
rahisi kuresha mkopo huo.
“Sisi walimu ukitaka kujua mimi
nalipwa shilingi ngapi ni rahisi tu kwa kuwa mishahara ya serikali mara nyingi
inajulikana hasa pale mtumishi unapoenda kukopa mahali ndio maana tunaiomba
serikali itusaidie kukopa viwanja kuwa kuwa tunauwezo wa kulipa kwa awamu tatu”
alisema Kimbale
Aidha Kimbale aliwatupia lawama
maafisa elimu na walimu wakuu wa shule kwa kuwanyima ruhusa bila kuwa na sababu
maalum.
“Wakurugenzi amekuwa ametoa kibali
upewe ruhusa lakini viongozi waliochini ya mkurugenzi wanatuwekea vipingamizi
ambavyo havieleweki kitu kinachozua utata mkubwa baina ya viongozi na walimu
ambao sio viongozi” alisema Kimbale.
mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri Williamuakizungumza na waandishi wa habari wakati wa mkutano mkuu wa chama cha walimu Tanzania (CWT) wilaya ya Mufindi mkoani Iringa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...