KAMPUNI ya mafuta ya Puma
Energy leo imekabidhi hundi yenye thamani Tsh milioni 25 kwa waandaaji wa mbio
za Rock City Marathon ikiwa ni mwendelezo wa kampuni hiyo kudhamini mbio hizo
zinazotarajiwa kufanyika Octoba 29 mwaka huu, Uwanja wa CCM Kirumba jijini
Mwanza.
Akikabidhi hundi hiyo kwa
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya mbio hizo Bw Zenno Ngowi, Meneja Mkuu
wa kampuni ya Puma Energy Bw Phillipe Corsaletti alisema udhamini
huo unalenga kuunga mkono juhudi za serikali kuhamasisha michezo na utalii wa
ndani hapa nchini.
“Michezo huleta uimara
wa afya na uimara huo ndio umetufikisha Puma Energy hapa tulipo kimafanikio. Ni
wazi ushiriki wa Puma kwenye mbio hizi utawajaza nishati ya nguvu na ubora
washiriki wote’’ alisema.
Aliahidi kuwa kampuni
yake itaendelea kushirikiana na waandaaji wa mbio hizo katika kuboresha zaidi
mbio hizo kwa miaka ijayo huku akitoa wito kwa vijana wengi zaidi
kutoka mikoa mbalimbali kujiandaa kwa ajili ya mbio hizo.
Akizungumza baada ya
kupokea hundi hiyo, Ngowi alisema uwepo wa kampuni hiyo katika kufanisha Rock
City Marathon utaongeza hadhi na ubora wa mbio hizo ili ziende sambamba na
ubora wa huduma na bidhaa zinazoandaliwa na kampuni hiyo.
Naye, Mratibu wa mbio
hizo kutoka kampuni ya Capital Plus International (CPI), Bw. Bidan Lugoe
alisema pamoja na medali washindi wa kwanza wa mbio za kilomita 42 kwa
wanaume na wanawake watajinyakulia sh. Mil 4 kila mmoja, Sh mil 2/- kwa
washindi wa pili na sh. Mil 1/- kwa washindi wa tatu.
Mkurugenzi
Mkuu wa kampuni ya Puma Energy Bw Phillipe Corsaletti (kushoto)
akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya sh milioni 25 kwa Mwenyekiti
wa Kamati ya Maandalizi ya mbio za Rock City Marathon Bw Zenno Ngowi (wa
tatu kushoto) ikiwa ni udhamini wa mbio hizo wakati wa hafla fupi ya
makabidhiano iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Wengine ni pamoja na
Meneja Masoko wa Kampuni ya Puma Energy Bw Machumani Shebe (wa tatu
kulia) na Mratibu wa mbio hizo kutoka kampuni ya Capital Plus
International (CPI), Bw. Bidan Lugoe (kulia)
Meneja Masoko wa Kampuni ya Puma Energy Bw Machumani Shebe (kushoto) akizungumza kwenye warsha hiyo.
Mwenyekiti
wa Kamati ya Maandalizi ya mbio za Rock City Marathon Bw Zenno Ngowi
(katikati) akizungumza kwenye warsha hiyo. Pamoja na mambo mengine Ngowi
alisema uwepo wa kampuni ya Puma katika kufanisha Rock City Marathon
utaongeza hadhi na ubora wa mbio hizo ili ziende sambamba na ubora wa
huduma na bidhaa zinazoandaliwa na kampuni hiyo.
Mratibu
wa mbio hizo kutoka kampuni ya Capital Plus International (CPI), Bw.
Bidan Lugoe akizungumza kuhusiana na maandalizi ya mbio hizo ambazo
pamoja na medali washindi wa kwanza wa mbio za kilomita 42 kwa wanaume
na wanawake watajinyakulia sh. Mil 4 kila mmoja, Sh mil 2/- kwa washindi
wa pili na sh. Mil 1/- kwa washindi wa tatu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...