Meneja wa Rasilimali Watu wa Radio Uhuru, Paul Mung’ong’o akizungumza baada ya kukabidhi msaada wa vitu mbalimbali katika Kituo cha Watoto wenye Kansa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili vyenye thamani zaidi sh. Milioni Mbili leo ambavyo vimetolewa na watu wanaosikiliza radio hiyo kupitia kipindi cha Kugusa Maisha yao.
Mwenyekiti wa Kamati ya Radio Uhuru na Mtangazaji wa Kipindi cha Gusa Maisha Yao, Joy Njarabi akizungumza juu ya uendeshaji wa kipindi hicho na kuweza kupata watu ambao wanaguswa moja kwa moja na kutoa msaada ikiwemo kwa kituo cha watoto wenye Kansa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Wafanyakazi wa Radio Huru wakiwa na watoto wa kituo hicho wakati wa kukabidhi msaada wa vitu mblimbali katika kituo hicho kupitia kipindi cha Gusa Maisha Yao.
Picha mbalimbali za wafanyakazi katika kituo cha watoto wenye Kansa


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...