Wanafunzi wakifurahia msaada waliopewa kwa kunyosha juu vifaa vya kujifunzia 

Na MWandishi Wetu
Shirika lisilo la kiserikali la Rise charity limezindua kampeni iitwayo Mtoto kwanza Elimu ni Msingi Ambapo kampeni hiyo yenye dhumuni la kusaidia watoto wa shule za msingi kwa kuwachangia vifaa mbalimbali vitakavyo wawezesha katika Masomo . 
Kampeni hiyo imezinduliwa kwa mara ya kwanza katika mkoa wa Morogoro wilaya ya kilosa kijiji cha Ngoisani ndani ya shule ya Mabwegere ikiwa ni kampeni inayotarajiwa kuzunguka katika mikoa mbalimbali Tanzania. 

Aidha wakati wa uzinduzi huo ulioambatana na kutoa msaada wa vifaa vya kujifunzia Katibu wa kampeni hiyo Atley Timothy Kayuni amewaasa watoto kwa kusema
"Msaada huu umetolewa na watanzania na wapenda maendeleo hivyo muutumie vizuri na kwamanufaa ya upataji elimu bora ambayo itawasaidia mbeleni katika maisha hivyo mkazane ili kutimiza ndoto zenu" amesema Kayuni.

Naye Mmoja wa walimu katika shule hiyo Mwl. Mbapila amelishukuru shirika hilo kwa kuwakumbuka na kwenda kuwaona na kusema ni watu wachache sana wenyemoyo wa kujitolea hivyo wasichoke kutoa kwani shule ni nyingi na nyingi zinahari mbaya hususani vijijini.
 Katibu wa kampeni ya "mtoto kwanza elimu ni msingi" Atley T Kayuni akitoa somo kwa wanafunzi wa shule ya msingi Mabwegere iliyopo Kilosa Mkoani Morogoro kabla yakutoa msaada kwa wanafunzi hao.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Rise Media, Innocent Horomo akitoa msaada wa vifaa vya kujifunzia kwa wanafunzi, ikiwa ni kampeni inayoendeshwa na Rise Charity iliyofanyika katika shule ya shule ya Mabwegere wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro.
 Afisa habari wa Rise Media ambae pia ni mwakilishi wa Rise Charity akiteta jambo na wanafunzi wa shule ya msingi mabwegere wakati wa zoezi la uzinduzi wa kampeni ya Mtoto kwanza elimu ni msingi
 Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Mabwegele wakiwa darasani wakati wa zoezi la kampeni ya Mtoto kwanza elimu ni msingi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Safi sana RISE CHARITY kwa kazi nzuri,,, hakika mungu atatenda jambo juu yenu kwa maana kazi mliyoifanya ni mfano mzuri wa kuigwa.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...