NA
K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, MADABA.
WANANCHI
wa Halmashauri ya mji wa Madaba, mkoani Ruvuma, wameipongeza serikali kwa
kuwafikishia umeme kwenye eneo lao ambapo wamesema utabadilisha maisha yao.
Pongezi
hizo zimetolewa Oktoba 11, 2017, kufuatia kukamilika kwa kazi ya kujenga njia
ya kusafirisha umeme kwenye eneo hilo ikiwa ni pamoja na kuweka mtandao wa
nyaya (wiring), kwenye eneo hilo na kwenye nyumba za wananchi kazi iliyokwenda sambamba na
ufungaji wa transofoma pozo.
Kwa
sasa Serikali kupitia Shirika lake la Umeme, TANESCO inatekeleza mradi mkubwa
wa umeme wa Makambako-Songea ambao unahusisha ujenzi wa njia ya kusafirisha
umeme wa msongo wa kilovolti 220Kv
Transmision Lines na usambazaji umeme vijijini (Rural electrification), katika
vijiji vya mkoa wa Njombe na Ruvuma ikiwa ni pamoja na kujenga vituo viwili
vipya vya kupoza umeme, huko Madaba na Songea na upanuzi wa kituo kingine mjini
Makambako.
“Nimefurahi sana eneo letu kupata umeme, kwa muda
mrefu sana tumekuwa tukitegemea umeme wa solar, sasa nina matumaini makubwa
nimeona kazi zinavyoendelea hapa za kuweka nguzo za umeme, kutandaza nyaya
majumbani na kuweka transofa, na tumeambiwa tukae mkao wa kula kwani umeem
utawaka muda wowote kuanzia hivi sasa.” Anasema
Rehema Maluwa, (pichani juu).
Nyumba zikiwa na madishi ya tv kwenye Halmashauri ya mji wa Madaba mkoani Ruvuma ambazo bila shaka kwa muda mrefu wamekuwa wakitumia fedha nyingi kutokana na matumizi ya jenereta kupata umeme lakini ujio wa umeme wa TANESCO utapunguza gharama za uendeshaji.
Maendeleo ya ujenzi wa msingi wa kufungia mashine kituo cha Madaba, ukiendelea Oktoba 11, 2017.
Maendeleo ya ujenzi wa msingi wa kufungia mashine kituo cha Madaba, ukiendelea Oktoba 11, 2017.
Mafundi wa TANESCO kwa kushirikiana na mkandarasi kutoka kampuni ya India ya Kalpataru, wakiwa kwenye eneo la ujenzi wa minara ya kupitisha laini za umeme wa 220kV huko Iboya, Njombe.
Mafundi wa TANESCO kwa kushirikiana na mkandarasi kutoka
kampuni ya India ya Kalpataru, wakiwa kwenye eneo la ujenzi wa minara
ya kupitisha laini za umeme wa 220kV huko Iboya, Njombe.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...