Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni ya Azam Media akizungumza na waandishi akiwaeleza waandishi wa Habari , namna watanzania watakavyopata nafasi ya kuangalia mashindano ya Cecafa moja moja, baada ya kuingia mkataba na Cecafa kufanya hivyo. Kulia kwake ni Mkuu wa uzalishaji wa vipindi Charles Hillar, na kushoto ni meneja Mauzo na Masoko John Mbele.
Na Karama Kenyunko, Globu ya jamii.
Shirikisho la vyama vya soka Afrika Mashariki na Kati, (Cecafa), limeingia mkataba na kampuni ya Azam Media kuonyesha mechi zote za Kombe la Challenge mwaka huu zinazotarajiwa kuanza kutimua vumbi mapema mwezi ujao.
Akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi mtendaji wa Azam, Tido Mhando amesema mkataba Huu utawezesha watanzania kupata uwezo mkubwa wa kandanda na pia tunataka kupata uwezo mkubwa zaidi na kusaidia kifanikisha soka ya Tanzania.
"Bado tunadhamira kubwa ya kuhakikisha ari hii inasambaa hadi katika nchi za jirani, mara nyingi tunakuwa tunajilaumu kuwa hatujapiga hatua, tunataka kuhakikisha tunakuwa chachu ya mafanikio" amesema Mhando.
Amesema, watatoa matangazo yao katika mashindano hayo ambayo ni kongwe zaidi nchini kuliko mengine yotote kwa lugha ya kiswahili na kiingereza na hata kwa lugha mbali mbali hasa hasa Rwanda na Uganda.
"Watanzania wajiandae kupata burudani ya kutosha na inayowastahili kwa kuhakikisha tunawafikishia matangazo yetu ya Cecafa Challenge kwa ubora wa hali ya juu. Aidha amesema wanamatumaini makubwa kuwa timu za Tanzania na Zanzibar
Zitafanya vema na hatimae kufudhu katika hatua za fainali na mshindi atabaki nchini..
Ameongeza kuwa hawataishia kwenye mashindano ya Cecafa tu, watafanya maonyesho makubwa katika mashindano ya Kagame cup." Naomba tushirikiane ili kuhakikisha mashindano haya yanapata hadhi yake inayostahili.
Mashindano ya Cecafa yanatarajiwa kuanza kutimua vumbi nchini Kenya kuanzia Desemba 3 katika viwanja vya Machakos na Kakamega huku timu tisa zikitarajiwa kushiriki baada ya timu ya Zimbabwe kujitoa.
Timu zitakazoshiriki ni Kenya, Rwanda Libya, Tanzania, Zanzibar, Uganda, Burundi, Ethiopia na S.Sudan
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...