Na Nteghenjwa Hosseah, Kibaha.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Selemani Jafo amemtaka atakayepewa jukumu la ukarabati wa Shule ya Sekondari ya Ruvu wilayani Kbaha mkoa wa Pwani wafanye kazi kwa kasi na haraka ili kuboresha mazingira ya shule hiyo. 
Jafo aliyasema hayo leo asubuhi katika shule ya sekondari Ruvu iliyopo mkoani pwani ambapo ni siku ya pili tokea shule  zianze kufunguliwa kwa mwaka huu 2018. Waziri Jafo alitumia siku ya kwanza ya tarehe 08 January ya kufunguliwa shule hapa nchini kwa kuongea na wanafunzi wa mkoa wa mbeya kupitia shule ya sekondari Ilomba iliyopo jiji la Mbeya.
Jafo amesisitiza kwamba Serikali imeamua kufanya ukarabati wa Shule zote kongwe hapa nchini kupitia TEA ili kutengeneza mazingira bora ya kujifunzia na kufundishia. 
Amesisitiza kwamba Serikali inayo ongozwa na Rais Dkt. John Magufuli imedhamiria kuleta mapinduzi makubwa katika elimu hapa nchini.
Jafo amewaeleza wanafunzi na walimu wa Ruvu sekondari kwamba wakati wa zoezi la ukarabati atatumia muda mwingi kukagua ujenzi wa shule hiyo akiwa pamoja na mbunge wa Jimbo hilo Mhe. Hamood Abuu Jumaa ili thamani ya fedha ipatikane.
Wanafunzi wa Ruvu sekondari walionyesha furaha kubwa kwa mipango ya Serikali juu ya shule yao kwani uchakavu wa miundombinu umekuwa ukiwaletea shida kubwa kutokana na maeneo mengi ya majengo yao kuvuja wakati wa Mvua.
 
Pia walimu na wanafunzi wa Shle hiyo wameahidi matokea mazuri zaidi katika mitihani inayokuja kwa kuzingatia mangira bora ya kujifunzia na kujisomea watakayokuwa wameyapata baada ya Ukarabati huo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selamani Jafo akikagua miundombinu ya Shule ya Sekondari ya Ruvu wakati alipotembelea shule hiyo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selamani Jafo akikagua mambweni ya  Shule ya Sekondari ya Ruvu wakati alipotembelea shule hiyo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selamani Jafo akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Ruvu wakati alipotembelea shule hiyo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selamani Jafo  katika picha ya pamoja na walimu wa Shule ya Sekondari ya Ruvu wakati alipotembelea shule hiyo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selamani Jafo akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Ruvu wakati alipotembelea shuleni hapo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...