Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan amewataka  Watanzania kuchana na  vitendo vya uharibifu wa mazingira kwa lengo la kujiepusha  na athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi.

Mama Samia amesema hayo leo jijijini Dar es Salaam wakati wa ziara yake ya kutembelea miradi ya ujenzi wa kuta za kingo katika Bahari ya Hindi eneo la Ocean Road na Kigamboni.

Amesema kuwa Tanzania imeharibu mazingira yake kwa kiasi kikubwa hali inayofanya sehemu kubwa ya maeneo yote kuwa na hali tofauti na tulivyotegemea.Ametoa mfano Mji wa Dodoma ambao watu wamekata miti yote na hivyo kusababisha eneo hilo kuwa jangwa kiasi cha kusababisha maafa pindi mvua zinaponyesha.

Ametaja kuwa  mikoa mingi ambayo iliyokuwa na baridi sasa hivi imekuwa ikiongoza kwa joto sawasawa na mikoa iliyopo Pwani kwa mfano mikoa ya Kilimanjaro kila ukiangalia utabiri wa hali ya hewa unaambiwa ina nyuzi joto 32 hadi 33, kiasi ambacho awali haikuwahi kufikia hapo. Amesema adhabu yote hiyo na  athari zinazoonekana sasa inatokana na uharibifu huo mkubwa wa mazingira unaofanywa na baadhi ya wanachi kwenye maeneo mbalimbali nchini .

“Napenda kutumia mfano anaotumia Papa Francis kuwa ukimkosea mwanadamu utakwenda kulia kanisani au Msikitini utasamehewa lakini ukiyakosea mazingira hayana Msikiti wala Kanisa yatakuadhibu mpaka utakaporudi kuwa rafiki tena,"amesema Makamu wa Rais .

Ameongeza kuwa "Nasi tumeharibu mazingira kwa kukata miti, kuchimba mchanga katika fukwe na matokeo yake bahari imepata nguvu ya kula ardhi yetu,hivyo turekebishe tulipoharibu ili kurudisha urafiki huu".Amesema kwa Mkoa wa Dar es Salaam wakazi wake wamekuwa wakitupa taka katika mitaro na ikiziba inaleta madhara ya mafuriko, hivyo hiyo ni hasara kwa Taifa kwa kuwa tunatumia muda mwingi kutoa pole na anayepewa pole hutegemea uende na chochote umsaidie kama mahindi na fedha. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...