Mwenyekiti wa Michezo ya Jumuiya za majeshi ya Afrika ya Mashariki, Brigedia Jenerali Martin  Kemwanga amesema kuwa mashindano ya baiskeli yanajenga umoja kwa nchi za afrika Mashariki. 

Kemwanga ameyasema hayo alipokuwa anawakabidhi bendera ya nchi za Afrika Mashariki pamoja na kutangaza mshindano ya baiskeli yatayofanyika April 13 Mjini Zanzibar na Kumalizika wilayani Masasi mkoani Mtwara, amesema kuwa mashindano hayo kwa kauli mbiu ya Amani na Usafi wa Mazingira yanajenga umoja kati ya nchi wanachama. 

Amesema kuwa mashindano hayo yamekuja wakati wa mwafaka wa kutangaza fursa ya viwanda kwa nchi zitazoshiriki mashindano hayo pamoja na kutangaza umoja na  pamoja na  wananchi kuingia kwenye nchi hizo bila vikwazo vya aina yoyote. 

Rais wa Chama cha Mchezo wa Baiskeli Tanzania, Godfrey Mhagama amesema kuwa katika mashindano hayo nchi zitazoshiriki za Afrika Mashariki ni Tanzania ambaye ndie mwenyeji ,Kenya , Uganda , Rwanda , Burundi pamoja na Sudan Kusini na nchi wa Waalikwa ni Zambia na Ufaransa na nyingine zitajitokeza. 

Amesema kuwa wadau wa wajitokeze katika kufadhili mashindano hayo kwani muda bado wa kutosha ili waweze kufanikisha mashindano
Mwenyekiti wa Michezo ya Jumuiya za majeshi ya Afrika ya Mashariki, Brigedia Jenerali Martin  Kemwanga  akizungumza na waaandishi wa habari mara baada ya kuwakabidhi viongozi bendera ya Jumuiya ya Afrika ya Mashariki kwa ajili ya mashinano ya mchezo wa baiskeri yatakayofanyika nchini Tanzania.
Mkurugenzi Mtendaji wa Afrika Mashariki Fest, Kisembo Ronex Tendo akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mashindano ya baiskeri yatakayofanyika nchini Tanzania ili kuhamasisha Amani kwenye nchi za Afrika Mashariki.
Rais wa Chama cha Mchezo wa Baiskeli Tanzania, Godfrey Jax Mhagama akizungumza na kuhusu ujio wa nchi mbalimbali za Afrika mashariki kwenye mashindano ya Baiskeri yatakayofanyika nchini Tanzania
Mwenyekiti wa Michezo ya Jumuiya za majeshi ya Afrika ya Mashariki, Brigedia Jenerali Martin  Kemwanga akimkabidhi bendera ya Jumuiya ya Afrika ya Mashariki kwa Rais wa Afrika Mashariki Fest "Tanzania Chapter", Peter Nzunda wakati wa mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Picha ya Pamoja 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...