Hussein Makame-NEC
WAGOMBEA
27 wa ubunge na udiwani wameteuliwa kugombea nafasi hizo katika
uchaguzi mdogo utakaofanyika Februari 17, mwaka huu katika majimbo mawili ya
ubunge na kata nne.
Katika
uteuzi huo uliofanyika mwishoni mwa wiki, mgombea udiwani kupitita CCM katika kata ya
Kimagai iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya
Mpwapwa mkoani Dodoma, amepita bila kupingwa.
Mbali
na uteuzi huo, Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi katika kata sita za Tanzania
Bara wanatarajia kuteua wagombea wa udiwani wa kata hizo siku ya Jumatano ya
tarehe 24 Januari, 2018 kukamilisha kata 10 zilizopangwa kushiriki Uchaguzi
Mdogo wa Februari 17, 2018.
Akizungumzi
uteuzi huo, Kaimu Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)
Hamis Mkunga amesema mgombea huyo wa CCMa amepita bila kupingwa baada ya mgombea
wa CHADEMA kushindwa kurejesha fomu za uteuzi.
Amesema
katika uteuzi wa wagombea Jimbo la Kinondoni, msimamizi wa uchaguzi wa jimbo
hilo amewateua wagombea 12 ambao ni ambao ni Godfrey Maliza kutoka chama cha TLP, Johnson Mwangosya (SAU) na Mwajuma Milambo kutoka UMD.
Mkunga
amewataja wagombea wengine walioteuliwa kuwa ni John January Mboya (Demokrasia Makini), Maulidi Mtulia (CCM), na Mary
Mpangala wa DP.
Wengine
ni Salim Mwalimu (CHADEMA), Rajabu Salum
(CUF), Mohamed Majaliwa (NRA), George Christian (CCK), Ally Omari Abdallah (ADA THADEA) na Ashiri
Kiwendu wa AFP
Kuhusu
uteuzi wa wagombea ubunge katika Jimbo la Siha mkoani Kilimanjaro, Mkunga amewataja
wagombea wanne walioteuliwa kuwa ni Dk Godwin Mollel (CCM) Mdoe Azania Yambazi (SAU),
Tumsifuheri Mwanry (CUF) naElvis Christopher MosiwaCHADEMA.
Katika
kata tatu zilizobaki, Mkunga amevitaja vyama vya siasa vilivyopitisha wagombea
ambao waliteuliwa katika kata ya Isamilo iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya
Nyamagana mkoa wa Mwanza kuwa ni Chama cha CUF, DP, UDP, CCM, na CHADEMA.
Amevikumbusha
vyama na wagombea kuheshimu maadili ya uchaguzi katika kipindi hiki cha kampeni
kwani vyama vyote vimekubaliana kuheshimu maadili hayo na kuwaomba wananchi
wajitokeze kwa wingisiku ya kupiga tarehe 17 Februari mwaka 2018.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...