Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainabu Telack amefanya ziara ya kukagua kilimo cha zao la Pamba na Mtama wilayani Kishapu kwa ajili ya kuendelea kuhamasisha wakulima kulima mazao hayo kwa wingi kwa njia za kitaalamu ambayo yatawafanya wakue kiuchumi na mkoa kwa ujumla. 

Telack amefanya ziara hiyo leo Jumatatu Januari 8,2018 wilayani Kishapu kwa kukagua baadhi ya mashamba ya pamba na mtama ambayo yamelimwa na wakulima kwa njia ya kitaalamu na kuwataka wakulima kuendelea kutii magizo ya serikali kwa kulima mazao hayo ya biashara na chakula ambayo yatabadili mfumo wa maisha yao pamoja na kuacha kuishi kwenye nyumba za tembe.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara baada ya kutembelea mashamba ya wakulima katika kijiji na kata ya Shangihilu Telack amewataka wakulima kijijini kuendelea kujikita kulima mazao hayo ya pamba na mtama kwa njia ya kitaalamu ambayo itawafanya kupata mavuno mengi na kuinuka kiuchumi. 

“Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na rais wetu mpendwa Dkt. John Pombe Magufuli imejipanga kumuinua mkulima kiuchumi kupitia kilimo na ndiyo maana changamoto zote zilizokuwa zikimkabili mkulima zinatatuliwa ili muweze kunufaika na kilimo chenu , hivyo nawasihi mlime mazao ya pamba na mtama kwa wingi kwani soko lake lipo”,alisema Telack. 
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainabu Telack mwenye ushungi akiwa na mkuu wa wilaya ya Kishapu Nyabaganga Taraba (katikati mwenye nguo ya njano) na aliyepo mkono wa kushoto ni Diwani wa Kata ya Shangihilu Mohamed Hamadi pamoja na wataalamu wa kilimo na mkurugenzi wa halmashauri hiyo Steven Magoiga wakikagua shamba la pamba hekali 22 la mkulima Kazimiri Masunga -Picha na Marco Maduhu- Malunde1 blog
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainabu Telack akiwa katika shamba la pamba na viongozi mbalimbali
Mkulima wa zao la Pamba Kazimiri Masunga akimuonyesha mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainabu Telack ukubwa wa eneo alilolima shamba hilo hekali 22, na kutarajia kwenye mavuno kumuinua kiuchumi huku akiomba serikali kuwapatia dawa ya kuua wadudu waharibifu ili wasipate hasara.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainabu Telack akiangalia wadudu wanavyolishambulia zao hilo la pamba na kutoa maagizo kuhusu ufumbuzi upatikane wa kuwateketeza kwa kupulizia dawa yenye nguvu ya kuua wadudu ili kutowapatia hasara wakulima.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...