Serikali imetoa miezi
sita kwa wananchi wanaolima ndani ya eneo la hifadhi ya reli inayopita Wilaya
ya Kilosa mkoani Morogoro kuhama eneo hilo baada ya kuvuna mazao yao ili
kuhifadhi miundombinu ya reli na kupunguza uharibifu wa miundombinu hiyo.
Hayo yameelezwa na
Naibu Waziri wa uchukuzi na Mawasiliano wa Wizara ua Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye wakati wa ziara yake alipotembelea
kukagua ukarabati wa reli iliyopo eneo la Kilosa, Morogoro na Gulwe, Dodoma
lenye umbali wa kilomita mia moja baada ya kuharibika kwa mvua na Serikali
kusitisha usafirishaji wa abiria na mizigo kutoka Dar es Salaam kwenda mikoa
mbali mbali na nchi za jirani.
Nditiye amesema kuwa
uharibifu wa eneo hilo ni wa kiwango kikubwa kwa kuwa katika kipande cha umbali
wa kilomita mia moja zilizoharibika kwa mvua baadhi ya maeneo reli imebomoka,
kuhama kwenye njia yake na ardhi husika kuliwa na maji ya mvua yaliyojaa kwenye
mto Mkondoa ambao unapita pembezoni mwa reli hiyo.
Ameongeza kuwa
uharibifu huo unasababishwa na shughuli za kibinadamu ambapo wananchi wanaishi
na kulima ndani ya mita thelathini upande wa kulia na kushoto mwa reli ambapo
ni hifadhi ya miundombinu ya reli na wananchi hawaruhusiwi kutumia eneo hilo
kwa shughuli yeyote.
Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye akipanda kiberenge kwenda kukagua ukarabati wa reli iliyoharibika kwa mvua katika eneo la umbali wa kilomita mia moja lililopo kati ya Kilosa, Morogoro na Gulwe, Dodoma.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania, Bwana Masanja Kaodogosa (wa pili kulia) akimuonesha Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (wa kwanza kulia) kazi ya kukarabati reli ikiendelea unaofanywa na wafanyakazi wa Shirika hilo baada ya kuharibika kwa mvua wakati wa ziara yake ya kukagua ukarabati huo katika kijiji cha Mkadage kilichopo wilayani Kilosa mkoani Morogoro.
Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye akishuka kwenye tingatinga inayojaza udongo kwenye eneo lililopo katika kijiji cha Munisagala kilichopo wilayani Kilosa mkoani Morogoro baada ya kukagua kazi inayoendelea ya kujenga na kurejesha miundombinu ya reli iliyoharibika na mvua wakati wa ziara yake kwenye eneo hilo. Katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania Bwana Masanja Kadogosa.
Kazi ya kujaza udongo kwenye eneo la ukubwa wa mita 170 lililopo katika kijiji cha Munisagala kilichopo wilayani Kilosa mkoani Morogoro ikiendelea kwa ajili ya kujenga na kurejesha miundombinu ya reli iliyoharibika na mvua.
Mhandisi Mkuu Ujenzi wa TRL Mhandisi Nelson Ntejo akimuonesha Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano (kulia) uharibifu wa miundombinu ya reli uliotokea kutokana na mvua wakati wa ziara yake ya kukagua uharibifu huo na ukarabati unaoendelea kati ya Kilosa, Morogoro na Gulwe, Dodoma. Katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania Bwana Masanja Kadogosa.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...