Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu Acacia kupitia migodi yake ya Buzwagi na Bulyanhulu imekabidhi hundi za shilingi bilioni 1.1 kwa halmashauri ya wilaya ya Mji wa Kahama na Msalala mkoani Shinyanga kwa ajili ya malipo ya ushuru wa huduma kwa kipindi cha Mwezi Julai hadi Disemba mwaka 2017. 

Acacia imekabidhi hundi ya shilingi milioni 924,881,819.78 kwa halmashauri ya wilaya ya Mji wa Kahama zilizotolewa na mgodi wa Buzwagi na hundi ya shilingi milioni 153,591,456 kwa halmashauri ya wilaya ya Msalala zilizotolewa na mgodi wa Bulyanhulu na kufanya jumla kuwa shilingi bilioni 1.1. 

Meneja Mkuu wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu,Benedict Busunzu amekabidhi hundi hizo kwa mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurulu leo Alhamis Februari 8,2018 mjini Kahama. 
Katikati ni Meneja Mkuu wa Migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu akikabidhi hundi ya shilingi153,591,456 kwa Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu kwa ajili ya malipo ya ushuru wa huduma kwa halmashauri ya wilaya ya Msalala katika kipindi cha mwezi Julai hadi Disemba 2017. Kulia ni Meneja wa Huduma na Mahusiano wa Acacia, Elias Kasitila 
Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu akikabidhi hundi hiyo ya shilingi milioni 153 kwa Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Msalala Simon Berege 
Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkuru,Meneja mkuu wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu,Meneja wa Huduma na Mahusiano wa Acacia, Elias Kasitila na Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Msalala Simon Berege wakiwa wameshikilia hundi ya shilingi milioni 153. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...