Mkurugenzi Mtendaji TANESCO Dkt. Tito Mwinuka, ametembelea kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Ibadakuli, kilichopo Mkoani Shinyanga.
Katika ziara hiyo, Dkt. Mwinuka amejionea shughuli mbalimbali zinazofanyika kituoni hapo.
Kituo hicho ni mojawapo ya vituo vilivyofanyiwa upanuzi wakati wa utekelezaji wa Mradi wa njia ya Kusafirisha umeme ya msongo wa kilovolti 400 (Backbone) kutoka Mkoani Iringa hadi Shinyanga.

Mkurugenzi Mtendaji TANESCO Dkt. Tito Mwinuka, akisaini Kitabu cha Kumbukumbu ya Wageni Wakati alipotembelea kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Ibadakuli, kilichopo Mkoani Shinyanga.

Muonekano wa kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Ibadakuli, kilichopo Mkoani Shinyanga.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...