Meneja wa Bia ya Castle Lager, Pamela
Kikuli, akionyesha moja ya kipeperushi kinachoelezea mashindano maalumu ya soka yanayofahamika kama ‘Castle Lager
Africa 5s’ (5 – Aside) yaliyozinduliwa leo katika viwanja vya Leaders, Kinondoni jijini Dar es salaam. Kulia ni Meneja
Masoko, Udhamini na Promosheni za Wateja George Kavishe na kushoto ni Mkufunzi wa Timu ya Castle Lager Tanzania, Ivo Mapunda.
Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia kinywaji chake cha Bia ya
Castle Lager, imezindua rasmi mashindano maalumu ya soka yanayofahamika kama ‘Castle Lager
Africa 5s’ (5 – Aside). Mashindano haya yenye hadhi ya kimataifa yanashirikisha timu za wachezaji watano (5) kila upande,
na kocha mmoja. Mechi zake zitakuwa zikichezwa kwa dakika saba (7) ili kata mshindi.
Bingwa wa michuano hiyo ataiwakilisha Tanzania huko Zambia katika michuano ya kimataifa dhidi ya
nchi nyingine 5 kutoka Afrika ambazo ni: Afrika Kusini, Zambia, Zimbabwe, Swaziland, Lesotho.
Baada ya hapo mshindi atapata fursa ya kwenda Urusi kushuhudia michuano ya Kombe la Dunia
baadaye mwaka huu, akiambatana na mashabiki wawili ambao watapatikana katika mchakato
malumu pamoja na mchezaji mmoja mkongwe kutoka nchi ambayo ni bingwa. Kama Tanzania
itafanikiwa kushinda, timu pamoja na mashabiki hao wawili wataongozana na mkongwe katika soka
Ivo Mapunda aliyekua kipa wa Taifa Stars na Simba Sports Club.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Meneja wa Bia ya Castle Lager, Pamela
Kikuli, alisema kuwa, kuna michakato maalumu ya kupata timu shiriki kupitia katika baa mbalimbali
jijini Dar es Salaam.
“Utaratibu wa kupata timu utawahusisha moja kwa moja mashabiki wa baa husika kupendekeza timu
zao, kabla ya hatua nyingine za kuzipigia kura timu zinazotakiwa kushiriki. Mteja wetu atapata
maelekezo maalumu kutoka kwa watu wetu ambao watakuwa wakipita katika baa hizo kwa nyakati
tofauti. Sifa kubwa ya mteja wetu kushiriki katika mchakato huo ni pamoja na kununua bia ya Castle
Lager,” alisema Kikuli.
Akitolea maelezo za ziada jinsi mchakato huo wa Castle Lager Africa 5s utakavyokua, Meneja
Masoko, Udhamini na Promosheni za Wateja George Kavishe amesema kua, michuano hiyo
inashirikisha baa 160, zitakazogawanywa katika makundi 10, huku kila kundi likiwa na baa 16. Kila
kundi litatakiwa kuwa na kiwanja chake katika michuano ya awali ya timu 16 na kupata timu 8.
Wilaya
zote za Mkoa wa Dar es Salaam zitashiriki katika michuano hii. Hapa tukimaanisha Kinondoni, Ilala,
Temeke, Ubungo na Kigamboni. Bonanza za kuanza kuchagua timu wakilishi za wilaya zitaanza
tarehe 17 Machi hadi 21 Aprili kisha Bonanza kuu itakayoleta timu 10 za fainali itakua tarehe 28 Aprili
2018.
“Katika hatua ya pili ya bonanza tutapata timu moja kutoka katika yale makundi 10 ya awali na
kufikisha idadi ya timu 10 zitakazocheza katika bonanza kubwa pale Viwanja vya Leaders jijini Dar es
Salaam, kupata timu tano (5) zitakazocheza kwa mtindo wa ligi na hatimaye kupata bingwa.” Alisema
Meneja Kavishe.
Michuano hii inafanyika kwa miezi miwili, ambapo washiriki wanatakiwa kuwa na umri wa miaka kati
ya 24 na 34. Lengo la mashindano haya ni kuwaleta pamoja marafiki na mashabiki wa soka.
Wachezaji walioko katika ligi mbalimbali nchini hawatoruhusiwa kushiriki katika michuano hii, hata
kama wana kigezo cha umri uliotajwa hapo juu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...