Mwenyekiti wa Wabunge wa Afrika Mashariki kutoka Tanzania Mheshimiwa Dkt Abdullah Hasnuu Makame (PhD) ameshiriki kama Mgeni Mashuhuri wa uzinduzi wa Kiti cha AXA cha Uchumi na Fedha katika Chuo Kikuu Cha London {School of Oriental and African Studies). AXA ni taasisi ya kifedha ya kimataifa yenye makao makuu yake nchini Uingereza; ambayo hivi Karibuni imebuni Kiti hicho kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha London kwa lengo la kufanya utafiti utakaowezesha miradi ya kupambana na umasikini katika Bara la Afrika. Kiti hicho kwa sasa kinakaliwa na Profesa Victor Murinde ambaye kabla ya hapo alikuwa Chuo Kikuu Cha Birmingham. Dkt Makame na Profesa Murinde Washachapisha makala mbalimbali za kitaaluma ya maeneo ya Uchumi na fedha katika majarida na makongamano mbalimbali.
 Kutoka kushoto ni Bi. Annabel Bligh Mhariri wa Biashara na Uchumi katika shirika la The Conversation UK, Hassan El-Shabrawishi Afisa Maendeleo wa Mikakati wa Afrika wa AXA, Bi Christine Oughton Profesa wa Utawala wa Uchumi  - SOAS - Chuo Kikuu Cha London, Mwenyekiti wa Wabunge wa Afrika Mashariki kutoka Tanzania Mheshimiwa Dkt Abdullah Hasnuu Makame. Bw Laurent Clavel Mkuu wa Divisheni ya Utafiti wa Uchumi  AXA, Profesa Victor Murinde, Mwenyekiti  wa AXA Uchumi na Fedha na Dkt George Kararach Mtafiti Mwandamizi wa Kamisheni ya Uchumi wa Afrika ya Umoja wa Mataifa UNECA
 Mheshimiwa Dkt Abdullah Makame akiwasilisha neno la uzinduzi wa Kiti akisikilizwa na Profesa Christine Oughton
 Mwenyekiti wa Wabunge wa Afrika Mashariki kutoka Tanzania Mheshimiwa Dkt Abdullah Hasnuu Makame akichangia mada. Pembeni yake ni  Dkt. Hassan El-Shabrawishi Afisa Maendeleo wa Mikakati wa Afrika wa AXA
 Mwenyekiti wa Wabunge wa Afrika Mashariki kutoka Tanzania Mheshimiwa Dkt Abdullah Hasnuu Makame akibadilishana mawazo na mmoja wa washiriki katika uzinduzi wa Kiti cha AXA cha Uchumi na Fedha katika Chuo Kikuu Cha London {School of Oriental and African Studies).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...