Na Karama Kenyunko, Blogu ya jamii.

Shahidi wa pili wa Upande wa Mashtaka katika kesi ya kutumia dawa za kulevya  inayomkabili msanii Wema Sepetu ameieleza  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa aliijaza fomu ya kupima sampuli ya mkojo wa Wema, kabla hajamfanyia vipimo.

Aidha Shahidi huyo, Inspekta Wille, alidai kuwa hajawahi kupeleka sampuli za mkojo  za washtakiwa Angelina Msigwa  na Matrida Seleman Abbas ambao ni wafanyakazi wa Wema kwenda kuchunguzwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kuhusu kukutwa na dawa za kulevya aina ya bangi.

Shahidi ameeleza hayo leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba alipokuwa akihojiwa na Wakili wa upande wa utetezi, Albert Msando baada ya kumaliza kutoa ushahidi wake.

Alipoulizwa muda gani alipeleka sampuli hiyo kwa Mkemia, alidai kuwa aliijaza fomu ya kupeleka sampuli ya mkojo wa Wema saa nne kamili asubuhi akiwa ofini kwao na kuandika maneno kuwa sampuli hiyo ya mkojo iko kwenye chupa ya plastiki lakini alikuwa bado hajampima mshtakiwa.

Alipoulizwa kama alijaza fomu hiyo kwa kuhisi tu, alidai, alijaza hivyo kwa kutumia uzoefu wake wa miaka 15 katika jeshi la polisi kwani alikuwa anajua taratibu za upimqaji ukifika katika ofisi ya Mkemia mkuu wa Serikali mkojo unakuwa katika chupa ya plastiki.

Aliendelea kudai kuwa Februari 8, mwaka jana alifika katika ofisi za Mkemia Mkuu wa Serikali  saa tano asubuhi na kumkabidhi Mchunguzi Elia Mulima kichupa cha plastiki ambacho ndani kilikuwa na mkojo.

Wakili Msando alimuuliza shahidi ulikuwapo wakati sampuli ya mkojo uliokuwamo ndani ya kichupa cha plastiki  unaodaiwa kuwa ni wa Wema ulipochukuliwa ambapo Inspekta Wille alidai kuwa hakuwapo.

Wakili Msando alimuuliza Inspekta Wille anaweza kusema kuwa unajua kwa uhakika kilichokuwa ndani ya chupa ya plastiki kuwa ni mkojo na je ni mkojo wa Wema? Alijibu kuwa hajui.

Msando alimuhoji Inspekta Wills kuwa walikaa kwa muda gani katika Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Inpekta Wille alidai kuwa hakumbuki.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...