Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
MFUMUKO  wa bei wa Taifa  wa Januari 2018 umebaki kuwa asilimia 4.0 kama ilivyokuwa mwezi Desemba 2017 kwa ujumla inamaanisha kuwa kasi ya mabadiliko ya bei ya bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia mwezi Januari 2018 imekuwa na kasi ilivyokuwa kwa mwaka. 
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na Jamii wa  Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS), Epharaim Kwesigabo amesema  kubaki kwa mfumko huo kunatokana na bidhaa na huduma kuendelea bei ileilie ya mwezi Desemba.
Amesema baadhi ya bidhaa za vyakula vilivyochangia kupungua kwa mfumuko wa bei huo ni  Mahindi kwa asilimia 8.0, Maharage 4.3. Ndizi ya kupika asilimia 9.0, Samaki kwa asilimia 9.0 kwa upande mwingine baadhi ya bei za bidhaa zisizo za Chakula zilizochangia mfumuko wa bei ya mwezi Januari 2018 ni pamoja na sare za shule kwa asilimia 2.3, Huduma za afya kwenye Hospitali Binafsi  kwa asilimia 10.0, Mkaa asilimia 9.4, Vitabu vya shule kwa asilimia 2.7 na gharama za malazi asilimia 3.2.
Kwesigabo amesema mfumuko wa bei nchini una mwelekeo unafanana na nchi nyingine Afrika Mashariki ambapo Kenya Mfumuko wa bei wa mwezi Januari 2018 umeongezeka hadi asilimia 4.83 kutoka asilimia 4.50 kwa mwaka ulioishia Desemba 2017, Uganda Mfumuko wa bei umepungua hadi kufikia asilimia 3.0 kutoka asilimia 3.3 kwa mwaka ulioishia wa mwezi Desemba 2017.
Aidha amesema Mfumuko wa bei wa Taifa unapima kiwango cha kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma zote zinazotumiwa na kaya binafsi nchini.
Kwesigabo amesema NBS ni Taasisi ya Umma  iliyoanzishwa kwa sheria ya kufanya uratibu upatikanaji wa takwimu rasmi.
 Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na Jamii wa  Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS), Epharaim Kwesigabo akizungumza na waandishi wa habari juu mfumuko wa bei wa Mwezi Januari 2018 leo jijini Dar es  Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...