JESHI la Polisi mkoani Kilimanjaro linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Hadija Msangi (30 ) mkazi wa Mwanzini  kwa tuhuma za kumchinja mtoto wake  mwenye umri wa miezi tisa na kitu chenye ncha kali shingoni hadi kufa .

Mtoto aliyeuawa ametambulika kwa jina la Hashim Msuya na kwamba mtuhumiwa baada ya kufanya unyama huo aliuweka mwili wa mtoto huyo kwenye mfuko wa Safleti na kuuhifadhi kwenye uvungu wa kitanda chake.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Kamishna Msaidizi wa Polisi ,Hamis Issah amethibitisha kutokea kwa tukio hilo mnamo Februari 26 mwaka huu majia ya saa 10:00 katika kata ya Msangeni wilaya ya Mwanga na kwamba tayari uchunguzi wa kidaktari umefanyika.

Na Dixon Busagaga wa Michuzi Media Group -Kilimanjaro.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...