Na Humphrey
Shao, Globu ya Jamii
Wakala wa
Usajili, Ufilisi na Udhamini(RITA) imefanya maboresho ya Kanzidata na mfumo wa
usajili wa vizazi na kifo kupitia mradi wa maboresho ya miundombinu ya Tekknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).
Akizungumza
na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam leo Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na
Sheria, Profesa Sifuni Mchome amesema kuwa lengo kuu la maboresho ni kuwezesha matukio
ya vizazi na vifo kufanyika kwa ufanisi zaidi na kuwa karibu na wananchi katika kuimarisha miundombinu ya usajili, krahisisha usafirishaji taarifa, uhifadhi wa taarifa
pamoja na matumizi ya taarifa za ndani na nje ya Wakala.
“Maboresho
ya mfumo wa usajili yamezingatia mahitaji ya mkakati wa kitaifa wa usajili wa
matukio muhimu ya binadamu wenye lengo la kuboresha usajili wa matukio muhimu”
amesema.
Amesema maeneo
yaliyolengwa katika mradi huo ni kama yafuatavyo ni kuboresha miundombinu ya
kanzidata , kuweka vituo 60 vya majaribio na madawati manne ya usajili wa RITA katika Makao Makuu , Maboresho ya mfumo wa kielektronikI wa usajili ,maboresho ya
mfumo wa utafutaji wa taarifa za zamani na kuweka mfumo maalum wa kutoa namba
za kuzaliwa.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Profesa Sifuni Mchome akizungumza na Waandishi wa Habari Juu ya mfumo mpya wa usajili wa Wakala wa Usajili, ufilisi na Udhamini (RITA) kwa kutumia TEHAMA wakati alipofanya ziara katika wakala huo leo jijini Dar es Salaam.
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili ,ufilisi na Udhamini (RITA), Emmy Hudson akitoa ufafanuzi juu ya mfumo wa usajili wa vizazi na vifo kupitia mradi wa maboresho ya Miundombinu wakati Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Profesa Sifuni Mchome alipofanya ziara katika wakala huo leo jijini Dar es Salaam.
Watendaji na Waandishi wa habari wakifatilia Mkutano wa Wakala wa Usajili, ufilisi na Udhamini (RITA) leo jijini Dar es Salaam.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...