Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii.

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeelezwa kuwa, msanii wa Filamu na Miss Tanzania mwaka 2006  Wema Sepetu  alimueleza askari polisi kuwa anatumia bangi kama starehe.

Shahidi wa tatu wa upande wa mashtaka, WP 6441 DC Mary (35) ameyaeleza hayo leo Februari 26 mwaka huu alipokuwa akitoa ushahidi wake katika kesi ya matumizi ya dawa za kulevya inayomkabili Wema na wafanyakazi wake wawili.

Akiongozwa na Wakili wa Serikali, Constantine Kakula mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, WP Mary amedai, Februari 4, 2017 alipewa maelekezo na mkuu wake wa kazi OC CID Denis Mujumba kumtoa Wema mahabusu na kwenda nyumbani kwake kufanya upekezi.

Amedai waliondoka  yeye, OC CID Mujumba, Inspekta Wille, Koplo Robert na DC Hassan na kuwa wkiwaa njiani alimuuliza Wema kuhusu tuhuma zinazo mkabili kama anahusika na uuzaji wa dawa za kulevya ama kutumia.

Shahidi huyo alieleza,  Wema alimjibu kuwa yeye hajishughulishi na uuzaji wa dawa za kulevya ila anatumia bangi kama starehe.Alidai kuwa alimuuliza Wema kuwa ni lini ilikuwa mara mwisho kutumia bangi  nakwamba siku hiyo ilikuwa Jumamosi ya Februari 4,mwaka 2017 na Wema alimwambia kuwa  Mara ya mwisho kutumia bangi ilikuwa siku ya Jumatatu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...