Na  Bashir  Yakub .


1.  NINI MAANA  YA  KUACHISHWA  KAZI  KIMAKOSA.     

Katika  ujumla  wake  kuachishwa  au  kufukuzwa  kazi  kimakosa ni  hatua  ambapo  mwajiri  anamwachisha  au  anamfukuza  kazi  mwajiriwa  wake  bila  kufuata  utaratibu  wa  sheria.  Mwajiri  asipofuata  sheria  katika  kumuondoa  mwajiriwa  kazini  ndipo  anapokuwa  amemiwachisha  kazi  kimakosa. 


Na  hapa  haiongelewi  Sheria  ya  ajira  na  mahusano  kazini  tu  inayotakiwa kuzingatiwa, bali  sheria  zote  ambazo  huhusika katika  ajira na mikataba  ikiwemo  sheria ya  mikataba  na  nyinginezo. Sheria yoyote   haipaswi  kuvunjwa  au  kukiukwa  wakati  mwajiriwa  anapotakiwa  kuachishwa  kazi.


2.   AINA  MBILI  ZA  KUACHISHWA  KAZI  KIMAKOSA.

Kuachishwa  kazi  kimakosa  kumegawanyika  mara  mbili ;

( a ) KUACHISHWA KWA KOSA AMBALO HALIPO(WRONGFUL TERMINATION).


Hii  ni  pale  ambapo  mwajiri  anamtuhumu  mwajiriwa  kwa  kosa  ambalo  hajatenda  kabisa.  Anamtungia  kosa  ili  amuondoe  kazini  kwasababu   anazojua  mwenyewe.  Au  inakuwa  ni  kweli  mwajiriwa  ametenda  kosa  lakini kosa  lile  halina  hadhi  au  uzito  wa  kumwondoa   kazini.  Sio  kila  kosa  ni  la  kumwondoa  mtu  kazini.  Makosa  mengine  ni  ya  kuonya  au  kuelekeza  tu. 


Kwahiyo  haya yakitokea  ndipo  tunaposema  kuwa mwajiriwa  ameachishwa  kazi   kimakosa.  Kimakosa  kwa  maana  kwa  kosa  ambalo  halipo  au  lipo  lakini  halitoshi  kumuachisha  mtu  kazi( not  justifiable).


( b ) KUACHISHWA KAZI KWA KOSA  AMBALO LIPO  LAKINI  BILA  KUFUATA UTARATIBU(UNFAIR TERMINATION).


Hapa  kosa  linakuwa  ni  kweli  kabisa  limetendwa.  Na  uzito  wa  kosa  lenyewe  unatosha  kabisa  kumuachisha mwajiriwa  kazi.  Tatizo  linakuja  kuwa  wakati  wa  kumuachisha  kazi  kwa  kosa  hilo  utaratibu  unakiukwa.  Kosa  sawa  lipo, lakini   utaratibu  wa  kutumia  kosa  hilo kumwondoa  mtu  ndio  uliokiukwa.


Utaratibu  ni  kama  kutopewa  taarifa(notice) , au kupewa  taarifa  lakini  katika  muda  usiostahili, kutolipwa  stahili, kutopewa  nafasi  ya  kusikilizwa, nk.  Kwahiyo utaona  tofauti  ya aina  hizi  mbili  za  kuachishwa  kazi  kimakosa.


Hata hivyo, pamoja  na  utofauti  huu bado  unachostahili  baada  ya  kuachishwa  kazi  kimakosa  ni  kilekile.  Aliyeachishwa  kwa  kosa  ambalo  halipo  na  aliyeachishwa  kwa  kosa  ambalo  lipo  lakini  kwa  kukiuka  utaratibu  wote  hustahili  stahili  sawa  kama  tutakavyoona hapa.


                           KUSOMA  ZAIDI  sheriayakub.blogspot.com


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...