Na Rhoda Ezekiel Kigoma,
MKUU wa Wilaya ya Buhigwe mkoani Kigoma, Kanali Marco Gaguti amewataka watendaji wa Serikali na wananchi kushirikiana katika shughuli za maendeleo katika ukusanyaji wa mapato na kufanya kazi.
Lengo ni kuboresha huduma za kijamii katika Wilaya hiyo na kuinua uchumi wa wananchi na Taifa kwa ujumla.Mwito huo aliutoa juzi katika chakula cha pamoja na wazee wa Wilaya ya Buhigwe ,Watumishi wa serikali, viongozi wa dini na chama pamoja na kuhamasisha shughuli za maendeleo.
Ambapo aliwataka kila mwananchi mmoja mmoja, kwa makundi na kwa ujumla wao kuweka mikakati ya pamoja ya kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya elimu, afya, miundombinu na jinsi ya kupatikana haki za wazee.
Mkuu huyo aliwataka watendaji wa Halmashauri kwa kushirikiana na wananchi wote ndani ya Wilaya kusaidia jitihada za kusukuma gurudumu la maendeleo kwa kusimamia vizuri ukusanyaji wa mapato."Lengo ni kuwezesha upatikanaji wa huduma za kijamii kwa mafanikio makubwa ambapo mapato hayo yatasaidia vijiji ambavyo havina zahanati vipate huduma hiyo kutokana na mapato hayo," amesema.
MKUU wa Wilaya ya Buhigwe mkoani Kigoma, Kanali Marco Gaguti akizungumza na Baadhi ya Watendaji wa Serikali na wananchi kushirikiana katika shughuli za maendeleo katika ukusanyaji wa mapato na kufanya kazi.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...