Na Agness Francis, Globu ya Jamii

KLABU Bingwa Afrika Mashariki na kati AzamFC inatarajia kuwakaribisha wachimba madini wa Shinyanga Mwadui FC katika michuano inayoendelea ya kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara. 

Mtanange huo utakao ni wa ushindani kwa kila timu kutaka kupata ushindi utafanyika kesho saa moja usiku na mchezo utachezwa katika Uwanja wa Azam Complex Chamazi jijini Dar es Salaam.

Azam FC wanatafuta alama 3 ili kuwakaribia Mabingwa watetezi Tanzania Bara  Yanga  wenye alama 40 wakiwa nafasi ya pili katika msimamo wa ligi hiyo.

Wakati Azam FC wakiwa nyuma kwa alama 35 na wapo nafasi ya tatu huku wakiongozwa na  vinara wa Ligi hiyo wekundu wa Msimbazi Simba  wakiwa na alama 46.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Ofisa Habari Azam FC Jaffary Iddy Maganga amesema kikosi kipo vizuri na wamejipanga kuchukua alama tatu wakiwa nyumbani.

"Tumeandaa timu vizuri na mwalimu  amepata muda wa kutosha wa kuandaa vijana  vizuri kuelekea mchezo huo na wachezaji wote walifanya mazoezi ya pamoja.

"Isipokuwa tutaendelea kumkosa mchezaji wetu katika mchezo wa kesho Yakubu Mohamed ambaye ni majeruhi"amesema Jaffary na kuongeza wanataka kubaki na alama tatu  kama ambavyo walizipata walipocheza na Singida United,"amesema Jaffary.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...