Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Emmanuel Kibona akitoa elimu ya
Kinga na Tahadhari Dhidi ya Majanga ya moto kwa Walimu na Wanafunzi wa Shule ya
Secondari Azania (Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji)
Na Nasibu Mgosso.
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ndicho chombo chenye jukumu la kuzuia na
kukabiliana na majanga mbalimbali kama mafuriko , Tetemeko la Ardhi,
ajali za vyombo vya usafiri na usafirishaji, kuporomoka kwa majengo,
migodi, pamoja na matukio ya moto.
Mara kwa mara, majanga ya moto yamekuwa yakitokea katika jamii yetu
kwa sababu moto ni sehemu ya maisha yetu ya kila siku. Utafiti
umethibitisha kwamba, vyanzo vingi vya moto ni sisi wenyewe
(binadamu) kutokana na uzembe, hujuma au kutokukuwa na elimu ya
Tahadhali na Kinga Dhidi ya Moto.
Aidha, matukio ya moto yamekuwa yakitokea mara kwa mara katika shule
za bweni hapa nchini hususani shule za sekondari, na kusababisha
uharibifu wa miundo mbinu kama vile Mali, majengo na wakati mwingine
majeraha au vifo kwa wanafunzi wetu na kuleta simanzi na sintofahamu
kwa Wananchi na Taifa kwa ujumla .
Picha ni sehemu ya bweni iliyoathirika na moto na kuteketeza mali za Wanafunzi.
Uchunguzi wa moto (Fire Investigation) umebaini sababu za matukio
hayo ni matumizi mabaya ya umeme yanayofanywa na wanafunzi kwa
kujiunganishia nyaya za umeme wenyewe bila kuwa na weledi iliwapate
sehemu za kuchaji simu na heater za kuchemshia maji kwa kificho kwa
sababu Wanafunzi hawaruhusiwi kuwa na simu wala heater pindi
wanapokuwa shuleni.
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...