Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Emmanuel Kibona akitoa elimu ya Kinga na Tahadhari Dhidi ya Majanga ya moto kwa Walimu na Wanafunzi wa Shule ya Secondari Azania (Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji)

Na Nasibu Mgosso. 

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ndicho chombo chenye jukumu la kuzuia na kukabiliana na majanga mbalimbali kama mafuriko , Tetemeko la Ardhi, ajali za vyombo vya usafiri na usafirishaji, kuporomoka kwa majengo, migodi, pamoja na matukio ya moto.

Mara kwa mara, majanga ya moto yamekuwa yakitokea katika jamii yetu kwa sababu moto ni sehemu ya maisha yetu ya kila siku. Utafiti umethibitisha kwamba, vyanzo vingi vya moto ni sisi wenyewe (binadamu) kutokana na uzembe, hujuma au kutokukuwa na elimu ya Tahadhali na Kinga Dhidi ya Moto.

Aidha, matukio ya moto yamekuwa yakitokea mara kwa mara katika shule za bweni hapa nchini hususani shule za sekondari, na kusababisha uharibifu wa miundo mbinu kama vile Mali, majengo na wakati mwingine majeraha au vifo kwa wanafunzi wetu na kuleta simanzi na sintofahamu kwa Wananchi na Taifa kwa ujumla .
Picha ni sehemu ya bweni iliyoathirika na moto na kuteketeza mali za Wanafunzi.

Uchunguzi wa moto (Fire Investigation) umebaini sababu za matukio hayo ni matumizi mabaya ya umeme yanayofanywa na wanafunzi kwa kujiunganishia nyaya za umeme wenyewe bila kuwa na weledi iliwapate sehemu za kuchaji simu na heater za kuchemshia maji kwa kificho kwa sababu Wanafunzi hawaruhusiwi kuwa na simu wala heater pindi wanapokuwa shuleni.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...