Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linapenda kutoa taarifa kwa umma kufuatia tukio la moto kwenye ukumbi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lililotokea mnamo tarehe 09 Aprili, 2018 majira ya saa 1:28 usiku mkoani Dodoma.

Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa moto huo ulisababishwa na shoti iliyotokana na Power bank iliyokuwa inatumiwa kuchaji simu. Shoti hiyo ilisababisha kuungua kwa simu, Power bank, sehemu ya meza na kapeti kitendo kilicholeta moshi mkubwa na taharuki miongoni mwa Wabunge. Ukiachilia mbali taharuki kwa Waheshimiwa Wabunge hakuna madhara kwa binadamu yaliyotokana na moto huo.

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji anatoa rai kwa Watanzania wote kuchukua tahadhari kubwa hasa wanapokua wanatumia vifaa vya kieletroniki ambavyo kwa sasa vipo katika matumizi hadi katika ngazi ya familia. Moto huzuka tu endapo kitapatikana chakula cha moto, joto la kutosha na hewa ya oksijeni (fuel, heat and oxygen).

Sambamba na hayo Kamishna Jenerali anahimiza uzingatiaji wa kinga na tahadhari ya moto katika maeneo yote. Wamiliki wa maeneo ya umma, binafsi na biashara wanapaswa kufunga vizimia moto kwa kuzingatia ushauri unaotolewa na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji lipo imara na litaendelea kuwaelimisha Watanzania kuzingatia kinga na tahadhari ya moto ili kuhakikisha maisha na mali vinakuwa salama. Imetolewa na;

CGF. Thobias Andengenye
Kamishna Jenerali
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
10 Aprili, 2018

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...