Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly ambaye alikuwaMgeni Rasmi katika Hafla ya Kitaaluma iliyo ambatana na Shukrani pamoja pongezi kwa mwanafunzi Bora kitaifa kidato cha Sita Bw. Anthony Mulokozi katika Shule ya Sekondari ya Mzumbe, Morogoro akitoa hotuba yake ambapo alimpongeza Anthony Mulokozi kwa kufanya vizuri, pia aliwapongeza walimu kwa kuendelea kuwa na juhudi za kuwafundisha wanafunzi kwa bidii na mwisho alisema kuwa juhudi zote hizi za elimu bora zinatokana na Serikali kuamua kulipa swala la elimu kipaumbele zaidi.
Mkuu wa Shule ya Sekondari Mzumbe Bw. Wenceslaus Mushi akielezea malengo ya Hafla hiyo ambayo ilikuwa ni ya kitaaluma zaidi na licha ya kuipongeza na kutoa Shukurani kwa Serikali lakini pia alimpongeza Tanzania One Anthony Mulokozi kwa kuwa Mwanafunzi Bora kidato cha sita kwa mwaka 2018 pamoja na wanafunzi wengine wote waliofanya vizuri pia aliwapongeza walimu kwa kuendelea kuwa na bidii ya kuwafundisha wanafunzi kwa weredi.
Afisa Elimu wa Shule za Sekondari Wilaya ya Mvomero Bw. Omat Sanga akizungumza neno wakati wa hafla hiyo ya kitaaluma iliyo ambatana na kutoa shukrani pamoja na pongezi katika Shule ya Sekondari Mzumbe .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...