Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

WAZIRI wa Habari,Sanaa,Utamaduni na Michezo Dk.Harrson Mwakyembe amewapongeza Nafasi Art Space kwa kutimiza miaka 10 tangu kuanzishwa kwake huku akielezea namna ambavyo wamekuwa wadau muhimu katika kukuza na kuendeleza sanaa za aina mbalimbali nchini.

Dk.Mwakyembe amewatembelea Nafasi Art Space katika ofisi zao zilizopo Mikochen B jijini Dar es Salaam akiwa ameambatana na Katibu Mtendaji ww Baraza la Sanaa Tanzania(BASATA) Godfrey Mngereza pamoja na viongozi wengine wa ngazi mbalimbali wakiwamo pia wa TAFCA.

Akiwa hapo Dk.Mwakyembe alipata nafasi ya kuelezwa historia ya Nafasi Art Space, mipango na mikakati ndani miaka 10 ya mwanzo.Mchoraji mahiri ambaye pia ni Mwalimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na mmoja ya wajumbe wa bodi na mwalinzi wa Nafasi Art Space Profesa Elias Jengo, alitumia nafasi hiyo kueleza mafanikio ya uwepo wao.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Nafasi, Rebecca amemueleza Waziri Mwakyembe kuwa Nafasi Art Space imefanikiwa kuipeleka mbele sanaa ya Tanzania na mkakati wao ni kuendelea zaidi ya hapo."Mkakati na malengo yetu ni kuipeleka sanaa mbele zaidi na kuongeza fursa na vipato vya wasanii kupitia sanaa," amesema.

Pia amezungumzia namna ambavyo wasanii wananufaika kwa studio za kufanyia kazi, mafunzo mbalimbali, nafasi ya kukutana na wasanii wenzao kupitia Nafasi Art Space.Pia fursa ya kukutana na wapenzi wa sanaa wanaoweza kuthamini kazi zao.Kuhusu mambo ambayo yamefanyika katika kuadhimisha miaka 10 ,Rebecca amesema Septemba mwaka huu wameshiriki shughuli mbalimbali za kijamii.



Waziri wa Habari,Sanaa,Utamaduni na Michezo Dk.Harson Mwakyembe akiangalia moja ya kazi ya uchongaji vinyago iliyofanywa na wasanii waliopo Nafaso Art Space baada ya kuwatembelea kwa lengo la kuwapongeza kwa kutimiza miaka 10.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...