Na Ahmed Mahmoud
Serikali imesema ipo mbioni kufunga kamera maalum (CCTV camera) kwenye miji na majiji mbalimbali nchini ili kudhibiti masuala ya uhalifu ikiwemo suala la utekaji unaofanywa na watu wasiojulikana.
Aidha Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yusuph Masauni amewaonya wanasiasa uchwara wanaotumia matatizo yanayotokea nchini kuacha mara moja tabia za kuisema serikali, taasisi na mashirika na wakiendelea watachukuliwa hatua. Masauni aliyasema hayo mapema leo Jijini Arusha wakati alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kata ya Murriet jijini Arusha katika ziara yake ya kukagua vituo vya Polisi ikiwemo kujua kama watuhumiwa wanapewa dhamana kwa saa 24 au la na masuala muhimu ya usalama.
Alisema kamera hizo zitafungwa kwaajili ya kubaini wale watekaji na watu wasiojulikana na kusisitiza kuwa ole wao wanasiasa wanaotumia matukio yanayotokea kwaajili ya kujipatia umaarufu wa kisiasa nchini. Alisema suala la ulinzi ni lazima lidhibitiwe haswa maeneo ya mipakani ili kudhibiti wale watu wenye nia ovu ndio maana hivi sasa mkakati wa serikali ni kufunga vifaa vya teknolojia ya kisasa zaidi.
“Hivi sasa serikali inamkakati wa kufunga kamera maalum kwaajili ya kudhibiti matukio ya kihalifu yanatokea katika miji na majiji na natoa onyo kwa wanasiasa kuacha kutumia suala la utekaji wa Mohamed Dewji kama mtaji wao waache vyombo vya dola zifanye kazi yake “ Pia alimwagiza Mkuu wa Polisi Wilaya ya Arusha,Almachius Mchunguzi kuhakikisha anatatua changamoto za kihalifu ikiwemo kutoa dhamana kwa washitakiwa kwa makosa yanatistahili dhamana ndani ya saa 24 na kulipobgeza Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha kupunguza uhalifu.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yusuph Masauni
Serikali imesema ipo mbioni kufunga kamera maalum (CCTV camera) kwenye miji na majiji mbalimbali nchini ili kudhibiti masuala ya uhalifu ikiwemo suala la utekaji unaofanywa na watu wasiojulikana.
Aidha Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yusuph Masauni amewaonya wanasiasa uchwara wanaotumia matatizo yanayotokea nchini kuacha mara moja tabia za kuisema serikali, taasisi na mashirika na wakiendelea watachukuliwa hatua. Masauni aliyasema hayo mapema leo Jijini Arusha wakati alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kata ya Murriet jijini Arusha katika ziara yake ya kukagua vituo vya Polisi ikiwemo kujua kama watuhumiwa wanapewa dhamana kwa saa 24 au la na masuala muhimu ya usalama.
Alisema kamera hizo zitafungwa kwaajili ya kubaini wale watekaji na watu wasiojulikana na kusisitiza kuwa ole wao wanasiasa wanaotumia matukio yanayotokea kwaajili ya kujipatia umaarufu wa kisiasa nchini. Alisema suala la ulinzi ni lazima lidhibitiwe haswa maeneo ya mipakani ili kudhibiti wale watu wenye nia ovu ndio maana hivi sasa mkakati wa serikali ni kufunga vifaa vya teknolojia ya kisasa zaidi.
“Hivi sasa serikali inamkakati wa kufunga kamera maalum kwaajili ya kudhibiti matukio ya kihalifu yanatokea katika miji na majiji na natoa onyo kwa wanasiasa kuacha kutumia suala la utekaji wa Mohamed Dewji kama mtaji wao waache vyombo vya dola zifanye kazi yake “ Pia alimwagiza Mkuu wa Polisi Wilaya ya Arusha,Almachius Mchunguzi kuhakikisha anatatua changamoto za kihalifu ikiwemo kutoa dhamana kwa washitakiwa kwa makosa yanatistahili dhamana ndani ya saa 24 na kulipobgeza Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha kupunguza uhalifu.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yusuph Masauni
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...