Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasilian0-Uchukuzi na Mawasiliamo Atashasta Nditiye  amezindua mkutano wa siku 3 wa wanatehama ili  kujadili masuala ya tehama na maendeleo ya viwanda nchini.

Nditiye amesema kuwa mkutano huo utawasaidia wananchi kutapata uelewa wa matumizi bora na usalama katika mitandao ya kijamii na amewataka wanatehama wote kutambulika na vyombo husika na wao kama serikali wanafanya kazi na watakaovuruga tasnia hiyo hatua kali dhidi yao zitachukuliwa.

Kwa upande wao kampuni ya Bussiness Connexion (BCX)  wanaojihusisha na masuala ya teknolojia ikiwa ni pamoja na kuuza bidhaa mbalimbali pamoja na komputa za aina zote  kutoka makampuni ya HP  na DELL, kutoa wataalamu wa kompyuta kwa makampuni, kutengeneza programu za simu na huduma za malipo wameshiriki semina hizo na kuwa kivutio kwa wadau wengi wa tehama.

Akizungumza na blogu ya jamii Afisa mauzo na masoko wa BCX  Justine Lawena amesema kuwa wameshiriki semina hiyo katika kujitangaza na kuonesha uwezo wao kwa serikali na wadau wa tehama na wao kama kampuni wana wataalamu wa kompyuta wakutosha  hivyo serikali na taasisi binafsi kutumia fursa hiyo.

Ameeleza kuwa katika kuendeleza sekta ya tehama wanatoa huduma za kuuza na kutengeneza mashine za kutoa pesa (ATM) na hadi sasa wanamiliki na kuendesha mashine zaidi ya 200 nchini.
 Afisa mauzo na masoko wa kampuni ya BCX  Justine Lawena akimkaribisha Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasilian0-Uchukuzi na Mawasiliamo Atashasta Nditiye  katika banda lao katika maonesho ya wadau wa tehama nchini.
 Afisa mauzo na masoko wa kampuni ya BCX Justine Lawena (kushoto) akitoa maelezo kwa mmoja wa wadau waliotembelea banda lao.
Afisa mauzo na masoko wa kampuni ya Bussiness connexion (BCX) Justine Lawena (kushoto) akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasilian0-Uchukuzi na Mawasiliamo Atashasta Nditiye wakati wa ufunguzi wa semina ya tehama kwa wadau.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...