Na Karama Kenyunko, Glogu ya jamii

ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) Wilaya ya Ilala, Norah Waziri maarufu kama Nora Mzeru amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala akikabiliwa na shtaka la kughushi cheti cha ndoa. 

Wakili wa serikali Mwandamizi, Ester Kyara amedai mbele ya Hakimu Mkazi, Flora Haule. 

Kwa kua katika siku isiyojulikana jijini Dar, es Salaam, kwa nia ya kudanganya, alighushi cheti cha ndoa chenye usajili namba 00040078 kwa nia ya kuonesha kuwa alifunga ndoa na marehemu Silvanus Mzeru Februari 4, 1995 katika kanisa la Roman Catholic la Mburahati wakati wakijua si kweli. 

Hata hivyo, mshtakiwa huyo baada ya kusomewa shtaka lake hilo, amekana na ameachiwa huru baada ya kutimiza masharti ya dhamana. 

Mahakama imemtaka mshtakiwa kuwa na wadhamini wawili wanaoaminika ambao watasaini bondi ya Sh 2milioni.  Kesi imeahirishwa hadi Novemba 21, mwaka huu.

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) Wilaya ya Ilala, Norah Waziri maarufu kama Nora Mzeru (Picha ya zamani).
Aliyekuwa  Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) Wilaya ya Ilala, Norah Waziri maarufu kama Nora Mzeru akiwa katika mahakama ya Wilaya ya Ilala leo akikabiliwa na shtaka la kughushi cheti cha ndoa. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...