Katibu, Ofisi ya Rais, Tume ya Utumishi wa Walimu, Winifrida Rutaindurwa amewashauri watendaji wanaojikita katika kutoa vitisho kwa walimu badala ya kutafuta mbinu bora za kuwasaidia kuacha kufanya hivyo ili Walimu wasijiingize katika makosa ya kinidhamu kwa kisingizio cha kuogopa vitisho.

Rutaindurwa ametoa kauli hiyo hivi karibuni jijini Dodoma alipokutana na Maafisa Elimu, Wathibiti Ubora, Waratibu Elimu Kata (Maafisa Elimu Kata), Walimu Wakuu na Wakuu wa Shule kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Lengo la mkutano huo lilikuwa kuwaelimisha Walimu Wakuu na Wakuu wa Shule kuzingatia  maadili na nidhamu kwa mujibu wa  Sheria, Kanuni, Taratibu pamoja na Miongozo mbalimbali inayotolewa na Serikali.

Alisema kuwa walimu hawapaswi kuishi kwa hofu kila wakati kutokana na vitisho wanavyopata kutoa kwa baadhi ya watendaji badala yake wanatakiwa kutekeleza majukumu yote kwa kuzingatia misingi na taratibu za utumishi wao.

Rutaindurwa alionesha kukerwa na baadhi ya watendaji wanaowasimamia walimu ambao kazi yao ni kutoa vitisho vya kuwafukuza kazi au kuwavua madakara endapo malengo flani hayatafikiwa bila kusaidia kutatua changamoto zinazokabili Walimu kufikia malengo.

“Unakuta mtu anakuambia wanafunzi wote wasipofaulu nakushusha cheo au nakufukuza lakini wala hamsaidii mkuu wa shule au mwalimu mkuu kutatua baadhi ya changamoto ambazo zipo ndani ya uwezo wake” alisema.

Aliongeza kuwa vitisho hivyo vimesababisha baadhi ya walimu kujikuta wakitenda makosa ya kinidhamu ili waonekane wamekidhi matakwa ya wanaowasimamia na matokeo yake wanachukuliwa hatua za kinidhamu ikiwemo kufukuzwa kazi.
 Katibu, Ofisi ya Rais, Tume ya Utumishi wa Walimu, Bibi Winifrida Rutaindurwa akitoa hotuba mbele ya Walimu Wakuu, Wakuu wa Shule, Maafisa Elimu Kata na Wathibiti Ubora (hawapo pichani) wa Manispaa ya Jiji la Dodoma katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Dodoma. Kulia ni Kaimu Katibu Msaidizi Wilaya ya Dodoma, Bibi Leticia Mwakasitu na Kushoto ni Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Bw. Abdallah Membe.
 Walimu Wakuu na Wakuu wa Shule wa Halmasahauri ya Jiji la Dodoma wakiwa katika hali ya furaha wakati wa Mkutano wao na Katibu, Ofisi ya Rais, Tume ya Utumishi wa Walimu, Winifrida Rutaindurwa ( hayupo pichani) uliofanyika jijini Dodoma.
 Walimu wakiwa katika hali ya utulivu wakimsikiliza Katibu, Ofisi ya Rais, Tume ya Utumishi wa Walimu, Winifrida Rutaindurwa (hayupo pichani) akiwaelimisha juu ya Sheria, Kanuni na Taratibu za Utumishi wa Walimu.
 Mmoja wa Walimu akiuliza swali kwa Katibu wa Ofisi ya Rais, Tume ya Utumishi wa Walimu, Winifrida Rutaindurwa (hayupo pichani) katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Dodoma.
 Mmoja wa Walimu akiuliza swali kwa Katibu wa Ofisi ya Rais, Tume ya Utumishi wa Walimu, Winifrida Rutaindurwa (hayupo pichani).
Mmoja wa Walimu akiuliza swali kwa Katibu wa Ofisi ya Rais, Tume ya Utumishi wa Walimu, Winifrida Rutaindurwa (hayupo pichani).

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...