NA BALTAZAR MASHAKA, MWANZA

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Nyamagana kimewavua uongozi Makatibu wa Siasa na Uenezi wa kata za Buhongwa na Mkolani wilayani humo kwa tuhuma na makosa ya kukidhalilisha na kukichafua kwenye jamii.

Pia kimelaani matukio hayo yaliyofanywa na viongozi hao wasio na hofu ya Mungu,katiba na sheria za nchi ambao wanakiangusha CCM kwa kufanya vitendo viovu na mambo ya ovyo yanayodhalilisha.

Akitoa tamko la kuwavua nyadhifa za uongozi makatibu hao wa Uenezi kwenye mkutano wa dharura wa Kamati ya Siasa ya Wilaya mbele ya vyombo vya habari Katibu wa CCM Wilaya ya Nyamagana Salum Kalli alisema viongozi wa namna hiyo hawatavulimiwa kwa sababu wanafedhehesha chama.

“CCM inalaani vikali mambo yaliyofanywa na viongozi hao kwenye jamii na hatua hii itakuwa fundisho kwa viongozi wenye tabia kama hizo,maana si utamaduni na maadili ya CCM kwani inawataka wawe waadilifu na waaminifu kwenye nafasi zao.Hivyo tutafuatilia tabia, mienendo na maadili ya kila kiongozi wa CCM aliyepo madarakani,”alisema.

Kalli alieleza kuwa Kamati ya Siasa ya Wilaya imechukua hatua hiyo na kutoa tamko hilo Watanzania wajue ili viongozi wenye tabia chafu zisizofaa kwenye jamii waache kwa kuwa CCM haitawavumilia.

Alifafanua kuwa Katibu wa Siasa na Uenezi wa Kata ya Buhongwa Hassani Bushagama, anadaiwa kumpa ujauzito mwanafunzi wa kidato cha tatu wa shule moja ambayo haikutajwa ambapo alitoroka na kutokomea tangu Julai mwaka huu.
Katibu wa CCM Wilaya ya Nyamagana Salum Kallia akisoma tamko la kuwavua uongozi makatibu wa Siasa na Uenezi wa kata za Buhongwa na Mkolani, Hassani Bushagama na Zephelin Maiko Shibugulu, mbele ya wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu wilayani Nyamagana jana.
Katibu wa CCM Wilaya ya Nyamagana Salum Kallia akisoma tamko la kuwavua uongozi makatibu wa Siasa na Uenezi wa kata za Buhongwa na Mkolani, Hassani Bushagama na Zephelin Maiko Shibugulu, mbele ya wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu wilayani Nyamagana jana.waliokaa mbele kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Zebedayo Athuman, Meya wa Jiji la Mwanza James Bwire na wa kwanza kulia ni Katibu wa Siasa na Uenezi Musptapha Banigwa
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Nyamagana, Zebedayo Athuman akifungua kikao kazi cha kamati ya siasa ya wilaya hiyo jana, kushoto ni Katibu wa Chama wilayani humo Salum Kalli na kutoka kulia wa kwanza ni Katibu wa Siasa na Uenezi Mustapha Banigwa na Meya wa Jiji la Mwanza James Bwire.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Nyamagana, Zebedayo Athuman akifungua kikao kazi cha kamati ya siasa ya wilaya hiyo jana, kushoto ni Katibu wa Chama wilayani humo Salum Kalli na kutoka kulia wa kwanza ni Katibu wa Siasa na Uenezi Mustapha Banigwa na Meya wa Jiji la Mwanza James Bwire. Picha na Baltazar Mashaka.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...