Jumuiya Kuu ya Watanzania nchini Uingereza inapenda kuwatangazia Watanzania wote na wana Africa Mashariki wanaoishi nchini Uingereza (UNITED KINGDOM) na IRELAND kuwa Sherehe za Uhuru Mwaka huu zitafanyika katika mji wa Luton siku ya Jumamosi tarehe 08/Desemba/ 2018 kuanzia saa mbili Usiku mpaka majogoo

Ifikapo saa sita usiku tutakuwa na tukio maalum litalofanywa na Mgeni rasmi pamoja wasanii maarufu wanaotegemewa kuwepo siku hiyo kukaribisha usiku wa tarehe 09/Desemba,  siku ya tuliyopata Uhuru 

Kutakuwa na kila aina ya vinywaji, nyama choma, chapatti’s, supu na mahanjumati ya kumwaga! 

Anuani ya Ukumbi

Lewsey Farm Learning Centre Executive Hall
92 Tomlinson Avenue
Luton
LU4 0QQ

Tiketi zinapatikana kupitia akaunti maalum ya Jumuiya kwa ajili ya kuadhimisha miaka 57 ya Uhuru

Kiingilio ni £20pp, Meza moja yenye kuchukua watu nane mpaka kumi ni £200, ili kujipatia tiketi yako deposit £20 kwa mtu mmoja au £200 kwa meza kisha Tuma ujumbe kwenda anuani Pepe tzukdiaspora@gmail.com

Akaunti maalum ya Jumuiya

Jina la Akaunti- UHURU
Bank - LLOYDS
Sortcode - 30 99 08
Akaunti No. 23619960

Burudani na sound system nzito itaporomoshwa na DJ DOUBLE T, DJ CHAMBI NA DJ ANDREW 

Hii si ya kukosa kwani kutakuwa na suprises za kumwaga, 

UHURU DAY TUKUTANE LUTON

Imetolewa na Jumuiya Kuu ya Watanzania UK

TZUK DIASPORA

08 DECEMBER 2018.

UMOJA NI NGUVU NA PAMOJA TUNAWEZA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...