*Yaomba radhi wasafiri, yafafanua utaratibu kusafirisha mazao ya misitu
*Pia yamzungumzia Ofisa wake wa Misutu, kumchukulia hatua za kinidhamu 


Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

WAKALA Wakala wa  Huduma za Misitu Tanzania (TFS)  umepokea taarifa kupitia mitandao ya kijamii na wadau  mbalimbali  zinazohusisha  namna  Ofisa  Misitu  wa Wilaya  ya  Korogwe mkoani Tanga ambavyo alikuwa akitekeleza majukumu ya kusimamia Sheria ya Misitu Na. 14 ya Mwaka 2002 pamoja na Kanuni
zake za  mwaka 2004.

Ofisa huyo  alikuwa akitekeleza  majukumu hayo kwa mujibu wa  kifungu cha 93 (Powers of officers with respect to offences) inayompa mamlaka Ofisa Misitu au Ofisa wa Jeshi  la  Polisi  kukagua,  kukamata  na  kuzuia  mazao  yanayodhaniwa  kupatikana  kinyume  na sheria.

Kwa kukumbusha tu leo kwenye mitandao ya kijamii kulikuwa na video inayosambaa kwa kasi kubwa ikionesha namna ambavyo wananchi wanalalamikia kitendo cha Ofisa Misutu akilumbana na abiria baada ya kulisamamisha gari na kubaini kuna vitanda vimebebwa.Hivyo kukaibuka malumbano ambayo yamechangia TFS kuamua kutoa ufafanuzi kwa vyombo vya habari.

Taarifa ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS) iliyotolewa leo Desemba 30,2018 imesema uongozi wa  TFS  umefanya uchunguzi wa haraka na kubaini  kuwa abiria mmoja  alikuwa akisafirisha  vitanda  viwili vipya  kwa  basi. Vitanda hivyo vililipiwa  ushuru wa Serikali kupitia mfumo wa Kielektroniki wa Malipo Serikalini (GePG) na kupewa stakabadhi halali ya Desemba 26, 2018 katika kituo cha Mkata, Handeni Mkoani Tanga.

Imefafanua katika kutekeleza  majukumu  yake,  Ofisa  wao alimtaka  abiria  huyo  kuonesha  hati  ya Kusafirishia  bidhaa  hizo  kwa  mujibu  wa  Kanuni  za  Misitu  Kifungu  cha  13, sehemu ndogo ya 4 ambayo inakataza mwenye chombo chochote  cha usafiri kusafirisha mazao ya  misitu  ambayo  hayana  hati  ya  usafirishaji  ambapo  abiria  huyo  hakuwa  nayo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...