Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na SHIVYAWATA wametoa mafunzo ya kuwajengea uwezo Wakurugenzi wa Sera na Mipango na Maafisa Utumishi Waandamizi juu ya masuala ya Watu wenye Ulemavu.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu wakati wa ufunguzi wa mkutano huo Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu Bw. Peter Kalonga amesema kuwa masuala ya Watu wenye Ulemavu ni mtambuka, hivyo ili kuifikia jamii jumuishi ni vyema kuhakikisha masuala ya wenye Ulemavu yanajumuishwa vyema katika mipango mkakati wa kila sekta.

“Sera ya Taifa ya huduma na maendeleo kwa Watu wenye Ulemavu pamoja na Sheria ya Watu wenye Ulemavu zinasisitiza ujumuishwaji wa watu wenye ulemavu katika nyanja mbalimbali za kijamii.” Alisema Kalonga. Aliongeza kuwa, Nchi yetu iliridhia Mkataba wa Kimataifa wa haki za Watu wenye Ulemavu wa mwaka 2006 unaotoa tafsiri ya mambo mbalimbali kuhusu haki za Watu wenye Ulemavu na kupelekea kutungwa Sheria ya Watu wenye Ulemavu Na. 9 ya mwaka 2010 ili kufanikisha utekelezaji wa mkataba huo na kukuza haki za watu wenye ulemavu nchini.
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi,Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Bw. Peter Kalonga akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo wakati wa mkutano wa kuwajengea uelewa Wakurugenzi na Maafisa Utumishi Waandamizi ngazi ya Wizara juu ya masuala ya Watu wenye Ulemavu yaliyofanyika Disemba 21 na 22, 2018 Jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu (SHIVYAWATA) Bi. Ummy Nderiananga akiwasilisha mada juu ya ujumuishwaji wa masuala ya Watu wenye Ulemavu.
Afisa Ustawi wa Jamii Mkuu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi,Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Bi. Josephine Lyengi akelezea jambo kuhusu ukondoishwaji wa masuala ya Watu wenye Ulemavu.
Baadhi ya washiriki wakimsikiliza hotuba ya Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi,Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Bw. Peter Kalonga (hayupo pichani).
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi,Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Bw. Peter Kalonga (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Wakurugenzi wa Sera na Mipango, Maafisa Utumishi Waandamizi na Wawakilishi kutoka Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu (SHIVYAWATA). PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...