Na Sultani Kipingo
Mwanafunzi Mtanzania anayesoma nchini China Isaack Ibrahim Emmanuel juzi ameibuka kidedea katika mchezo wa kick boxing baada ya kumpiga kwa KO Mchina Zi xiǎo yún yǔ katika Mjini Jillin.

Isaack, ambaye anasomea uhandisi wa Madawa (Pharmaceuticals engineering) katika Chuo Kikuu cha Liaoning jijini Shenyang, ameushangaza umati mkubwa wa Wachina baada ya kucheza kwa ustadi na hatimaye kumgaragaza Zi ambaye hajawahi kupigwa hata mara moja.

Mpambano huo wa Kg 60 umempa umaarufu mkubwa Isaack kiasi kwamba hata waandaaji wa mapambano wameanza kupigana vikumbo kumtaka acheze mapambano zaidi. Akiwa na uwezo wa kutumia kwa kasi ya ajabu miguu na mikono yote, wataalamu wa mchezo huo wamemtabiria makubwa kijana huyu wa kutoka Mwanza.

Akiongea na michuzi tv kwa njia ya mtandao, Isaack amesema yuko fiti kupambana na yeyote na popote huku akiendea na Masomo bila wasi.

Isaack Ibrahim Emmanuel akimenyana na Mchina Zi xiǎo yún yǔ katika Mjini Jillin.
Isaack Ibrahim Emmanuel akimpa kibano Mchina Zi Xiǎo Yún Yǔ katika Mjini Jillin.
Isaack Ibrahim Emmanuel akitangazwa mshindi dhidi ya Mchina Zi Xiǎo Yún Yǔ katika Mjini Jillin.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...