Kwa mwaka 2018 Mahakama ya watoto ya Kisutu ilipokea jumla ya mashauri 118 ya jinai na makosa 295 ya madai yalipokelewa na kufanyiwa kazi na matukio ya kesi za watoto yakiwa wengi wa watoto hao ni wale ambao wamekinzana na Sheria na pili ni wale ambao Sheria inawakuta na makosa. Hayo yamebainishwa na Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi wa Mahakama ya Kisutu Bi. Agness Mchome wa jijini Dar es Salaam wakati akitoa maelezo Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendelo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu Maendeleo ya Jamii) Dkt. John Jingu alipotembelea katika Mahakama ya Watoto Kisutu jijini Dar es Salaam.

Hakimu Agness Mchome amewataka wazazi kutimiza wajibu wao wa malezi kwa watoto ili kuwaepusha na mashitaka yanayozuilika kwani watoto wanaofikishwa mahakamani ni wale ambao wazazi au walezi wao hawakutimiza wajibu wao wa kutoa malezi stahiki.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendelo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. John Jingu ameridhishwa na utendaji kazi wa Mahakama ya Watoto ya Kisutu jijini Dar Es Salaam kwani imekuwa ikifanya kazi nzuri ya kusaidia kurekebisha maadili ya watoto nchini.

Dkt. Jingu amesisitiza wazazi kuzingatia malezi bora na kutoacha watoto kuangalia televisheni na mitandao ya kijamii wakati wote ambapo kwa kiasi kikubwa mitandao ya kijamii na video zisizo na maadili zinachangia kuharibu maadili ya watoto nchini.
 Katibu Mkuu Wizara yaAfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii) (kushoto) Dkt. John Jingu akisisitiza jambo wakati wa ziara yake ya kufuatilia utekelezaji wa kazi za Maendeleo na Ustawi wa Jamii na Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali katika Mkoa Dar es salaam (katikati) ni Afisa Ustawi wa Jamii Mwandamizi Bi. Rehema Kombe na kulia ni Afisa Ustawi wa Jamii wa mkoa wa Dar es Salaam Bi. Sufiani Mdolwa.
Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Dar es Salaam Bi. Given Sure (kulia) akitoa maelezo kuhusu utekelezaji wa kazi za Idara ya Maendeleo ya Jamii ya Mkoa kwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii) Dkt. John Jingu (hayupo pichani) na kulia ni Afisa Ustawi wa Jamii wa mkoa wa Dar es Salaam Bi. Sufiani Mdolwa. Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...