Mjumbe wa Bodi ya wakurugenzi ya baraza la kilimo Tanzania Bw Enock Ndondole akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wadau wa sekta binafsi katika kilimo, kwa niaba ya mwenyekiti wa Bodi, Mkutano huo umefanyika mkoani morogoro na kuhudhuliwa na wadau mbalimbali katika sekta ya kilimo.
Mkurugenzi wa Sera Baraza la Kilimo Tanzania Bw. Timothy Mmbaga akifafanua jambo wakati wa mkutano huo uliokuwa ukijadili mchango wao sekta binafsi katika utekelezaji wa mpango wa kuendeleza sekta ya kilimo nchini ASDP II.
Sehemu ya washiriki wa mkutano huo wa siku moja ulioandaliwa na Baraza la kilimo Tanzania na kufanyika Mkoani Morogoro.
Mkurugenzi Msaidizi wa sera na Mipango Wizara ya Kilimo Bw. Osward Ruboha,(wa kwanza) Makamo mwenyekiti Baraza la Kilimo Mh Jitu Son na Mjumbe wa Bodi wa Baraza la Kilimo wakifuatilia kwa makini mjadala uliokuwa ukiendelea katika Mkutano huo wa Sekta binafsi katika Kilimo.
Mkurugenzi Msaidizi wa Sera na Mipango Wizara ya Kilimo Bw. Osward Ruboha kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo.(Mwenye suti nyeusi kwa walioketi) akiwa katika Picha ya pamoja na wajumbe wa Mkutano wa Sekta binafsi katika Kilimo.


Baraza la kilimo Tanzania limewakutanisha wadau wa sekta binafsi katika kilimo ili kujadili mchango wao katika utekelezaji wa mpango wa kuendeleza sekta ya kilimo nchini ASDP II.

Mkutano huo wa siku moja umefanyika Mkoani Morogoro na kuhudhuliwa na wadau zaidi ya 60 wakiwemo maafisa wa Serikali, Taasisi za Kilimo na wadau wa Kilimo ambapo ulifunguliwa na Mkurugenzi Msaidizi wa sera na Mipango Wizara ya Kilimo Bw. Osward Ruboha kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...