Mshindi wa Biko jijini Dodoma, Hamad Ibrahim Ramadhan, amesema kwamba ameamua fedha zake za ushindi sh milioni 10 alizoshinda kutoka kwenye bahati nasibu ya Biko kumalizia ujenzi wa nyumba yake ili kuepuka adha alizokuwa anakutana nazo. 

Mshindi huyo alisema kwamba kabla ya fedha hizo, aliamua kuhamia kwenye nyumba yake yenye chumba kimoja akiishi na familia yake, jambo lililotatuliwa na ujio wa fedha za Biko nchini Tanzania. 

Naye mke wa mahindi huyo, Mwashabani Bakari Mwingi, aliishukuru Biko kwa kupunguza makali ya maisha yao kwa sababu nyumba yao itakamilika na wataanza kuishi maisha bora. 

Mama huyo alisema kuwa maisha ni magumu, hivyo mumewe kushinda Biko ni jambo la kumshukuru Mungu, maana hakuna aliyetarajia kwamba kuna siku watapata suluhu ya changamoto zao za kimaisha katika familia yao. 

Biko mchezo unaochezwa kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi unachezwa kwa kufanya miamala kuanzia sh 500 na sh 1000 na kuendelea, ambapo namba ya Kampuni ni 505050 na kumbukumbu namba ni 2456, huku washindi wa papo kwa hapo wakiibuka na kuanzia sh 5000 hadi sh milioni moja. 

Mbali na zawadi za papo kwa hapo, Biko inatoa ushindi mnono katika droo zake kubwa za Jumatano na Jumapili, ambapo washindi wake huibuka na mamilioni pamoja na bodaboda Ikiwa na lengo kubwa la kugawa utajiri kwa Watanzania wote.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...