Na Ripota wetu,Michuzi TV
KUNDI la matapeli linadaiwa kutumia jina la Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi nchini (NEC) Dk.Athumani Kihamia na kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.
Kututoka na utapeli huo Dk.Kihamia ametoa tahadhari kwa wananchi kuwa makini na utapeli unaoendelea kwenye mitandaoni wa kutumia jina lake.
Akizungumza kwa njia ya simu, Dk.Kihamia amesema kuna watu wamefungua akaunti feki ya face book na kuwatapeli watu kwa kuwatumia ujumbe kwa njia ya messenger.
"Kuna baadhi ya watu wamefungua akaunti kwa jina langu na kulitumia kwa kujipatia fedha kwa njia hiyo ya utapeli huku wakijua ni kosa kisheria ,"amesema.
Baadhi ya jumbe hizo ambazo zinatumika kufanyia utepeli zinasema kwamba Dk.Kihamia anauwezo wa kuwatafutia kazi katika mbuga ya Hifadhi ya Serengeti .
"Yaani tayari kuna watu wameliwa fedha na matapeli hao .Sehemu ya ujumbe huo unasema hivi "angalia kama kuna mtu amemaliza chuo na hajapata kazi uniambie maana kuna kazi shirika la Marekani la Thomson Zoology kule Serengeti National Park na wanahitajika watu wawili wenye diploma au degree kwa ajili ya kazi ya reservations na mshahara milioni moja na laki nane kama kuna mtu aniambie mapema nimoe namba ya huyo mzungu ahsante,"amefafanua wakati anaelezea utapeli huo .
Hivyo Dk. Kihamia amewataka wananchi kuwa makini na kwamba ujumbe uliko kwenye mitandao ya kijamii si wake ni wa matapeli.
"Nilishawahi kukanusha taarifa hiyo kupitia mitandao ya kijamii lakini naona hali inazidi kuendelea hivyo wananchi wanatakiwa kuupuuza ujumbe huo,"alisema Dk.Kihamia.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...