Huduma ya maombi na maombezi ya Radio safina jijini Arusha imeongoza mamia ya watu kutoka sehemu mbalimbali ndani na nje ya nchi ya Tanzania kushiriki katika kongamano la maombi maalum ya kuombea viongozi wa nchi ili waweze kuongoza nchi katika misingi inayompendeza Mungu.

Akizungumza na vyombo vya habari Makamu  Mkurugenzi wa huduma hiyo Bi.Hellen Lema amesema kuwa dhima kubwa ya maombi hao ni kuliweka taifa ya Tanzania katika kusudi na mpango wa Mungu utakaowafanya wananchi kunufaika na rasilimali walizonazo.

Aidha amesema kuwa maombi hayo ni maombi ya Esta ambayo yamelenga kusafisha njia kwaajili ya uchaguzi wa mwaka ujao ili uweze kufanyika kwa haki pasipo watu kugombana 

Kwa upande wake mtumishi Paschal Thomas ambaye ndiye aliyeongoza maombi hayo amesema kuwa kusudi la maombi hayo ni kuzuia mauti inayotengezwa na watu wasio na hofu na mungu hivyo wanatarajia baada ya maombi hayo kuona watanzania wa mataifa mengine kubadilika na kuenenda kama ambavyo mafundisho yao yanyofundishwa.

Naye mmoja wa wananchi Bernad ambao Kivuyo wamefika katika kongamano hilo amesema Bernard Kivuyo amesema kuwa wingi wa watu waliohudhuria katika viwanja hivyo anaamini kuwa Mungu anaenda kuwatoa sehemu moja kwenda nyingine kimafanikio.
Wananchi kutoka maeneo  mbalimbali ndani na nje ya Tanzania walio hudhuria katika kongamano la kuombea viongozi wa nchi ya Tanzania lililofanyika kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid Memorial Stadium Arusha

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...